Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari Mpya

Mlinda amani wa UNMISS akishika doria katika barabra karibu na Bentiu, jimbo la Unity, Sudan Kusini.
UNMISS Photo

Vikosi vya Umoja wa Mataifa Sudan Kusini vinawapeleka wanafunzi shuleni na kuwarudisha nyumbani wakati wa mitihani.

Walinda amani Sudan Kusini wasindikiza wanafunzi shuleni na kuwarudisha nyumbani wakati wa mitihani.Polisi waliopo kwenye ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini  wamepewa jukumu la kuwasindikiza wanafunzi hadi kwenye kituo cha mtihani kwenye mji mkuu wa Sudan Kusini, Juba.  Usindikizaji huo unafanyika Kwa wiki mbili ambapo askari hao wataendelea kuwapeleka na kuwarudisha wanafunzi kufanya mitihani yao kwa usalama.

Audio Duration
1'57"
Laurent Gbagbo na Charles Blé Goudé wakiwa mahakamani huko The Hague Uholanzi leo tarehe 15 Januari 2019 wakati hukumu ikisomwa. Wameachiwa huru.
ICC-CPI

ICC yawaachia huru Gbagbo na Blé Goudé

Mahakama ya kimataifa ya makossa ya jinai, ICC leo imemwachia huru rais wa zamani wa Côte d'Ivoire Laurent Gbagbo na aliyekuwa mkuu wa vijana Charles Blé Goudé baada ya upande wa mashtaka kushindwa kuthibitisha pasipo shaka mashtaka yote dhidi yao. Arnold Kayanda na taarifa zaidi.

Sauti
1'49"
Watoto  wakicheza  kwenye kwenye bomba la maji, kwenye eneo la shule iliyopo katika kambi ya ya wakimbizi wa ndani Bukasi huko Maiduguri nchini Nigeria.
UNICEF/UN055929/Gilbertson VI

Dola milioni 848 zahitajika kunusuru wakimbizi wa ndani kaskazini-mashariki mwa Nigeria

Nchini Nigeria, Kuongezeka kwa mapigano kati ya vikosi vya serikali na makundi yaliyojihami kaskazini mashariki mwezi uliopita wa Desemba na kumesababisha watu wengi zaidi kufurushwa makwao kutoka eneo la Baga na kuelekea kwenye kambi za wakimbizi wa ndani hujo Maiduguri na Manguno ambako tayari  kuna msongamano. John Kibego na taarifa zaidi.

Sauti
55"