Wasichana ni majaji watarajiwa, wafuate ndoto zao jamii ziendelee kunufaika - Hakimu Pamela Achieng
Mkutano wa 68 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake duniani, CSW68 ukiendelea hapa jijini New York Marekani tunavinjari hadi nchini Kenya kumsikia Hakimu Pamela Achieng ambaye azma yake ya kujikita kwenye masula ya kusimamia haki ilichochewa na swali alilojiuliza yeye mwenye ya kwamba “kama mwanaume anaweza kufanya kazi zinazotambulika hasa za kutetea haki za raia katika mahakama kwanini mwanamke asiweze?”