Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Pamela Achieng, Hakimu katika mahakama ya Ngong iliyo katika Kaunti ya Kajiado nchini Kenya.
UN News

Wasichana ni majaji watarajiwa, wafuate ndoto zao jamii ziendelee kunufaika - Hakimu Pamela Achieng

Mkutano wa 68 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake duniani, CSW68 ukiendelea hapa jijini New York Marekani tunavinjari hadi nchini Kenya kumsikia Hakimu Pamela Achieng ambaye azma yake ya kujikita kwenye masula ya kusimamia haki ilichochewa na swali alilojiuliza yeye mwenye ya kwamba  “kama mwanaume anaweza kufanya kazi zinazotambulika hasa za kutetea haki za raia katika mahakama kwanini mwanamke asiweze?”

 

 

Sauti
6'16"
Mamilioni ya watu kote ulimwenguni wanapoanza kuadhimisha mwezi Mtukufu wa Ramadhani, kwa huzuni huko Gaza na katika eneo lote, wengi wataadhimisha mwezi huu wakikabiliwa na migogoro, kufukuzwa na hofu.
© UNRWA

Ni wakati wa Ramadhan tusitishe uhasama Gaza na Sudan: Guterres

Leo ni mwanzo wa mwezi mktukufu wa Ramadhan ambapo Waislamu kote duniani hudumisha na kuchagiza tunu za amani, maridhiano na mshikamano lakini uhasama unaendelea hususani sehemu mbalimbali duniani ikiwemo Gaza ambako mauaji , na mashambulizi hayajakoma amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres akizungumza na waandishi wa habari mjini New York Marekani hii leo. 

Sauti
2'53"
Huduma za kibinadamu na haki za binadamu zazidi kutwama nchini Haiti..
© UNICEF/Ndiaga Seck

Haiti: Huduma za kibinadamu na haki za binadamu zazidi kutwama

Kutoroka gerezani kwa zaidi ya wafungwa 4,500 nchini Haiti mwishoni mwa wiki iliyopita wakiwemo viongozi mashuhuri wa magenge ya uhalifu kukitajwa kuwa tishio la usalama wa taifa, huku huduma muhimu kama afya, elimu zikiendelea kuzorota kila uchao, Umoja wa Mataifa unataka hatua za haraka za jamii ya kimataifa kuzuia taifa hilo kuzidi kutumbukia kwenye ghasia.

Mtoto mwenye umri wa mwaka 1 anafanyiwa unchunguzi wa matibabu kama kuna dalili za utapiamlo katika kituo cha mapokezi kwenye mpaka wa Sudan na Sudan Kusini.
© WFP/Hugh Rutherford

Uongozi wa jimbo la Upper Nile nchini Sudan Kusini waomba usaidizi zaidi wa ulinzi

Huku mzozo wa Sudan ukiendelea, wakimbizi na wanaorejea wanamiminika katika mipaka ya nchi jirani ya Sudan Kusini, wengi wamekuwa wakitafuta hifadhi katika jimbo la Upper Nile nchini humo na wanahitaji msaada wa haraka wa kibinadamu.  Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini UNMISS umefanya mazungumzo na uongozi wa jimbo hilo kuona namna ya kuwasaidia.

Sauti
2'25"
Dennis Francis, Rais wa kikao cha 78 cha Baraza Kuu, akitoa muhtasari wa vipaumbele vyake kwa 2024. (Maktaba)
UN Photo/Eskinder Debebe

Rais wa Baraza Kuu: Umoja wa Mataifa sio tatizo

Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa Dennis Francis Pamoja na mambo mengine amesema Umoja wa Mataifa "sio tatizo" bali tatizo linatokana na kwamba baadhi ya nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa wanahisi wanaweza kukiuka mkataba wa Umoja wa Mataifa watakavyo na kukiuka sheria za kimataifa bila kuadhibiwa.