Guterres alaani shambulio la Jumanne Soum, Burkina Faso
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres amelaani vikali shambulio lililotekelezwa Jumanne na kikundi cha watu waliokuwa wamejihami wasiojulikana huko kaskazini mwa Burkina Faso.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres amelaani vikali shambulio lililotekelezwa Jumanne na kikundi cha watu waliokuwa wamejihami wasiojulikana huko kaskazini mwa Burkina Faso.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres ameelezea kusikitishwa na ripoti za raia kuuwawa na wengine kutekwa na kundi la watu waliojihami kaskazini mwa jimbo la Borno kwenye eneo la Kaskazini Mashariki mwa Nigeria.
Shirika la mpango wa chakula duniani WFP na serikali ya Myanmar wametia saini makubaliano mapya kwa lengo la kutokomeza njaa. U Than Aung Kyaw, mkurugenzi mkuu katika idara ya mambo ya nje na Stephen Anderson mkurugenzi wa WFP nchini Myanmar ndio waliosaini makubaliano kati ya pande hizo mbili.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres ameelezea kusikitishwa na ripoti za raia kuuwawa na wengine kutekwa na kundi la watu waliojihami kaskazini mwa jimbo la Borno kwenye eneo la Kaskazini Mashariki mwa Nigeria
Mafunzo ya ufundi yaliyoanzishwa na Baraza la mashauriano na ubunifu mjini Bangui nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati CAR kwa kushirikiana na mpango wa Umoja wa Mataifa nchini humo MINUSCA yameleta neema kwa raia wa nchi hiyo.
Takriban wakimbizi 2,500 na wasaka hifadhi wanashikiliwa katika vizuizi nchini Libya kwa mujibu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR na Muungano wa Afrika AU.
Watoto wanaendelea kubeba gharama kubwa za machafuko yanayoshika kasi Kaskazini Magharibi mwa Syria limesema leo shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF.
Umoja wa Mataifa leo umeendelea kusisitiza kwamba kuhusu mauaji ya mwandishi wa Habari wa Saudia Jamal Khashoggi kinachotakiwa ni uchunguzi huru, usio na upendeleo ili kuhakikisha kuhakikisha uchunguzi kamili, na uwajibikaji, kwa ukiukwaji wa haki za binadamu uliofanywa katika kesi hiyo.
Umoja wa Mataifa umesema bado unawasiwasi mkubwa wa hatma ya usalama wa takriban raia milioni 3 huko Idlib Syria ambako zaidi ya nusu ya watu wote wametawanywa na kuwa wakimbizi wa ndani kufuatia ripoti za kuendelea kwa mashambulizi ya anga katika eneo hilo.
Kenya, Musumbiji na Niger wamezuia milipuko ya ugonjwa wa polio ambayo ilishuhudiwa nyakati tofauti katika kipindi cha miezi 24 iliyopita na kuchangia nchi hizo kutangazwa kuwa zisizokuwa na ugonjwa wa polio kwa mujibu la tangazo la shirika la afya duniani WHO lililotolewa leo.