WFP na serikali ya Myanmar wafanya ushirikiano mpya kutokomeza njaa
WFP na serikali ya Myanmar wafanya ushirikiano mpya kutokomeza njaa
Msaada wa Kibinadamu
Shirika la mpango wa chakula duniani WFP na serikali ya Myanmar wametia saini makubaliano mapya kwa lengo la kutokomeza njaa. U Than Aung Kyaw, mkurugenzi mkuu katika idara ya mambo ya nje na Stephen Anderson mkurugenzi wa WFP nchini Myanmar ndio waliosaini makubaliano kati ya pande hizo mbili.