Kamishna wa Haki za Binadamu wa UN ziarani nchini Ukraine
Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa Haki za Kibinadamu Volker Türk ameanza ziara ya siku nne nchini Ukraine hapo jana Jumapili Desemba 4 kwa mwaliko wa Serikali ya nchi hiyo akiwa ameongozana na wafanyakazi wa ofisi yake wanaohusika na kufuatilia masuala ya haki za binadamu.