Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Syria

Syria
OCHA Syria

Maelfu ya watu Maisha yao yanaendelea kuwa hatarini Syria:WHO/OCHA/UNHCR

Umoja wa Mataifa unaendelea kufuatilia kwa karibu hali inayotia hofu kubwa Kaskazini Magharibi mwa Syria kufuatia taarifa kwamba askari kadhaa wa Uturuki wameuawa kwenye shambulio la anga. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amerejelea wito wake wa kusitisha uhasama mara moja na kuokoa Maisha ya raia walio hatarini kufiuatia machafuko yanayoendelea na mashambulizi.

Sauti
2'22"
Wakimbizi wa Syria wakiwa mbioni kutafuta makazi
UNICEF/UN0277723/Souleiman

Mauaji ya raia na wimbi la watu kutawanywa lazima vikome Syria:UN

Mashambulizi ya angani na ardhini ya jimbo la Idlib Kaskazini Magharibi mwa Syria yanasababisha wimbi kubwa la watu kutawanywa na Maisha ya raia kupotea na haya ni madhila ambayo hayastahili na yanapswa kukomeshwa sasa amesema Geir Pedersen mwakilishi maalum wa Umoja wa Mataifa nchini Syria akitoa taarifa kwenye Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa hii leo.