Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Syria

Tarehe 11 Oktoba 2019 huko nchini Syria, mwanamke na wanae akiwa ameketi chini ya lori wakati huu ambapo wakimbizi wanawasili Ras al-Ain huko Tal Tamer, wakikimbia ghasia mpya kaskazini-mashariki mwa Syria.
© UNICEF/Delil Souleiman

WHO ina wasiwasi mkubwa kuhusu hali ya kaskazini mwa Syria

Shirika la afya duniani kuptia taarifa yake iliyotolewa mjini Cairo Misri, limeonesha wasiwasi mkubwa kuhusu hali ya afya ya binadamu kaskazini mwa Syria ambako watu takribani 200,000 wameyakimbia makazi yao kutokana na ongezeko la operesheni za kijeshi tangu Oktoba 9 na hivyo watu milioni 1.5 wako katika uhitaji mkubwa wa huduma za kiafya. 

Sauti
2'22"