Wauza silaha fuateni taratibu muepushe mapigano Afrika
Hivi karibuni katika mlolongo wa mijadala ya Afrika kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa kulifanyika mkutano wa siku moja kuhusu jinsi jamii ya kimataifa inaweza kukomesha milio ya bunduki barani Afrika, mkutano ambao ulihudhuriwa na wawakilishi wa nchi wanachama wakiwemo wabunge.