Uganda na uungaji mkono wa juhudi za UN za kuleta amani Somalia
Kikosi cha walinda amani 530 kutoka Uganda kipo nchini Somalia kwa ajili ya kusaidia kuleta amani na utulivu. Kikijumusha wanawake 63 na wanaume 467, kikosi hicho ni sehemu ya kikosi cha ulinzi cha Umoja wa Mataifa, UNGU, ambacho jukumu lake ni kulinda maeneo ya Umoja wa Mataifa kwenye mji mkuu Mogadishu ili kusaidia ujumbe wa umoja huo nchini Somalia, UNSOM na ofisi ya usaidizi wa Somalia, UNSOS ziweze kutekeleza mamlaka zao.