Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Somalia

Askari wa kike kutoka Uganda anayehudumu kwenye kikosi cha ulinzi cha Umoja wa Mataifa,  UNGU nchin Somalia akiwa na kitazama mbali wakati akiwa lindoni kwenye mji mkuu wa Somalia, Mogadishu
UN /Ilyas Ahmed

Uganda na uungaji mkono wa juhudi za UN za kuleta amani Somalia

Kikosi cha walinda amani 530 kutoka Uganda kipo nchini Somalia kwa ajili ya kusaidia kuleta amani na utulivu. Kikijumusha wanawake 63 na wanaume 467, kikosi hicho ni sehemu ya kikosi cha ulinzi cha Umoja wa Mataifa, UNGU, ambacho jukumu lake ni kulinda maeneo ya Umoja wa Mataifa kwenye mji mkuu Mogadishu ili kusaidia ujumbe wa umoja huo nchini Somalia, UNSOM na ofisi ya usaidizi wa Somalia, UNSOS ziweze kutekeleza mamlaka zao.

Maisha nchini Somalia kwa muda mrefu yamekuwa magumu kutokana na vita isiyokoma.
OCHA/Cecilia Attefors

Heko Somalia kwa mabadiliko ya kiusalama:UNSOM

Umoja wa Mataifa, Muungano wa Afrika, Muungano wa Ulaya, serikali ya Uingereza na serikali ya Marekani wamekatribisha hatua iliyochukuliwa na waziri mkuu wa Somalia Hassan Ali Khaire kuwaeleza wadau hao wa kimataifa kuhusu mabaddiliko katika sekta ya usalama nchini humo na miapango inachukuliwa na serikali kuendelea kuimarisha hali ya usalama Somalia.