Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa alaani mashambulizi ya kigaidi nchini Kenya na Somalia.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres kupitia taarifa iliyotolewa na msemaji wake hii leo jijini New York amelaani vikali shambulizi lililotekelezwa jana katika kaunti ya Wajir nchini Kenya ambapo takribani askari polisi nane wameuawa na wengine kujeruhiwa wakati gari lao lilipolipuliwa kwa kilipuzi kilichoundwa kienyeji.