Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Somalia

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres akiweka shada la m aua huko Christchurch New Zealand kuenzi waathirika wa shambulio la Machi mwaka huu.
UN /Mark Garten

Siku ya kimataifa ya waathirika wa matendo ya vurugu yanayotokana na dini au imani yaadhimishwa kwa mara ya kwanza.

Katika kuadhimisha siku ya kimataifa ya kuadhimisha waathirika wa matendo ya vurugu yanayotokana na dini au imani, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema ulimwengu unapaswa kupinga na kukataa wale ambao kwa mabavu na kwa uongo wanashawishi kujenga imani potofu, kuchochea mgawanyiko na kueneza hofu na chuki. 

Sauti
1'43"
Mwakilishi maalumu wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Somalia, James Swan akihutubia Baraza la Usalama.
UN Photo/Manuel Elías

Usalama wa Somalia bado ni wa wasiwasi, aonya Mkuu wa UNSOM

Katika hotuba yake ya kwanza kwa Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa mjini New York Marekani hii leo, mwakilishi maalumu wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Somalia, James Swan ameeleza hatua ilizozipiga Somalia katika kuboresha mambo kikatiba na kiusalama, miongoni mwa vipengele vingine, lakini akaonya kuwa mwanya wa kufikia hatua muhimu zaidi unazidi kuwa finyu.

Mtaalam huru wa haki za binadamu Somalia, Bahame Tom Nyanduga
UN Photo/Ilyas Ahmed)

Somalia bado inahitaji msaada wa kimataifa kupambana na changamoto za haki-Nyanduga

Mtaalamu huru wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya haki za binadamu nchini Somalia Bahame Tom Nyanduga akiwasilisha taarifa yake hii leo mjini Geneva Uswisi baada ya ziara yake mjini Mogadishu Somalia amesema, jumuiya ya kimayaifa inapaswa kuendelea kuisaidia Somalia kuimarisha taasisi zake na sekta ya sheria na usalama wakati huu wa kuelekea katika uchaguzi.