Chonde chonde wahisani tunawategemea sasa kuliko wakati mwingine wowote:UNICEF
Chonde chonde wahisani tunawategemea sasa kuliko wakati mwingine wowote:UNICEF
Henrietta Fore katika taarifa yake iliyotolewa leo mjini Geneva Uswisi amesema “sasa kuliko wakati mwingine wowote tunawategemea wahisani wetu kuendelea kusaidia kazi zetu kwa ajili ya kuwafikia wale wasio na chochote au yeyote licha ya kwamba huu ni wakati mgumu.”
Ameongeza kuwa ikiwa ni wiki moja tangu virusi vya Corona kutangazwa kuwa zahma ya kimataifa idadi ya visa inaendelea kuongezeka kote duniani. Pia amesema “mamilioni ya Watoto hawahudhurii shule, wazazi na watoa huduma wote wanafanyia kazi waliko inapowezekana, mipaka inafungwa na maisha yamepinduliwa. Na haya ni maji marefu kwetu sote”.
Ameongeza kuwa kwa upande wa UNICEf wanakabiliana na virusi hivi vipya vya corona, mila potofu na taarifa zisizo sahihi huku wakihakikisha usalama na afya njema kwa wamafanyazi wa shirika hilo na familia zao.
Amesisitiza kwamba “kazi yetu ya kuokoa maisha kwa kuwapa watoto afya njema, elimu, lishe na ulinzi sasa ni muhimu sana.”
Ukurasa kuhusu virusivyacorona & taarifa mpya
Wasomaji wanaweza kupata taarifa na muongozo kuhusu mlipuko wa virusi vya corona (2019-nCoV) kutoka Umoja wa Mataifa, Shirika la afya duniani na mashirika mengine ya UN hapa. Kwa habari mpya kila siku kutoka UN News, bofya hapa.Amesema wakati mamilioni wametawanywa, kuathirika na vita, kufa kutokana na magonjwa yanayoweza kuzuilika, kukosa masomo au kukosa chanjo muhomu, haja ya msaada ni kubwa sana.
Hivi sasa amesema UNICEF inafanya kila kila iwezalo kusaidia kuzuia kusambaa kwa virusi miongoni mwa jamii katika nchi zilizoathirika. “tunatoa taarifa sahihi kuhusu jinsi gani ya kuhkikisha familia ziko salama, kuwapa vifaa vya usafi na kujisafi mashuleni, vituo vya afya na kudhibiti athari za mlipuko kwa fursa ya watoto kupata huduma za afya, elimu na huduma za kijamii.