Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Burundi

Wanawake wakiteka maji katika mradi wa maji uliofadhiliwa na shirika la uhamiaji la Umoja wa Mataifa, IOM katika kambi ya wakimbizi wa ndani ya Dolow nchini Somalia. IOM, WFP na mashirika mengine waliweze kusaidia mahitaij ya wakimbizi hao kutokana na mfu
WFP/Georgina Goodwin

Kuchangia CERF ni uwekezaji bora zaidi- Guterres

Kuwekeza katika mfuko wa dharura wa Umoja wa Mataifa, CERF si tu kunafanikisha usaidizi wa kibinadamu bali pia ni kuwekeza katika kuboresha kazi za chombo hicho chenye wanachama 193, amesema Katibu Mkuu Antonio Guterres jijini New  York, Marekani hii leo wakati akifungua kikao cha ngazi ya juu cha kuchangia mfuko huo  ulioanzishwa mwaka 2006.

Waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa wa Burundi Ezechiel Nibigira akihutubia mjadala mkuu wa mkutano wa 74 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, UNGA74.
UN Photo/Cia Pak

Burundi yataka iondolewe kwenye ajenda ya Baraza la Usalama

Mjadala mkuu wa mkutano wa 74 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, UNGA74 ukitamatishwa hii leo  jiijni New York, Marekani, Waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa wa Burundi Ezechiel Nibigira amehutubia jukwaa hilo akitaka ajenda ya Burundi kwenye Baraza la Usalama iondolewe kwa kuwa hali ya usalama nchini humo ni tulivu.