Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Taarifa kuhusu Virusi vya Corona

Virusi vya Corona kama dharura ya afya ya umma:Taarifa za UN News Kiswahili
Mlipuko uliripotiwa mara ya kwanza Wuhan China Desemba 31, 2019

Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake  na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.

UN Women /Aidah Nanyonjo

Mimi kama mbunge ni wajibu wangu kuielimisha jamii jinsi ya kujikinga na COVID-19-Mbunge David Karubanga wa Uganda

Leo ni siku ya mabunge duniani ambapo mchango muhimu wa mabunge na wabunge unatambuliwa katika kuwawakilisha wananchi na kupaza sauti zao ili serikali imweke mwanajamii katika katika vipaumbele vyake inapoweka mipango ya nchi. Katika zama hizi za COVID-19, mabunge na taasisi nyingine za serikali nazo zimelazimika kwa kiasi fulani kufuata utaratibu mpya kujikinga na virusi ikiwemo kuweka umbali kati ya mtu na mtu na hata wakati mwingine kulazimika kufanya kazi nje ya majengo ya bunge kama ilivyo kawaida.

Sauti
3'39"
Winnie Byanyima ambaye ni mkurugenzi mtendaji mpya wa UNAIDS akiwa kwenye moja ya mikutano ya kuwawezesha wanawake kiuchumi kwenye Umoja wa Mataifa.
UN Photo/Amanda Voisard

Huduma ya afya haipaswi kuwa biashara bali haki ya binadamu:Byanyima 

Mkurugenzi mtendaji wa shirika la Umoja wa Mataifa linalopambana na ukimwi UNAIDS Winnie Byanyima amesema janga la corona au COVID-19 limeongeza adha kwa watu wanaoishi na VVU lakini pia kuyumbisha uchumi wa dunia na kuongeza pengo la usawa wa kijinsia, hivyo ameisihi dunia kuchukua hatua zinaozingatia haki za binadamu kama njia pekee ya kulidhibiti janga hilo.

Sauti
1'44"
© UNICEF

UNICEF yafikisha msaada wa COVID-19 kwa nchi zaidi ya 100 licha ya changamoto

Shirika la Umoja wa mataifa la kuhudumia watoto UNICEF limesema licha ya changamoto lukuki limefanikiwa kufikisha msaada kwa nchi zaidi ya 100 kupambana na janga la corona au COVID-19 na kuokoa maisha ya mamilioni ya watu. 

Katika ripoti yake iliyotolewa leo mjini New York na Copenhagen, UNICEF imesema wakati janga la COVID-19 likipindua maisha ya mamilioni ya watoto kote duniani , UNICEF inafikisha msaada wa kuokoa maisha licha ya kukabiliwa na vikwazo vingi na vikubwa ikiwemo masuala ya usafiri na matatizo ya kiufundi.

Sauti
2'10"
Mtoto akipokea dawa za TB nchini Sudan Kusini kwa msaada wa Global Fund kupambana na VVU,TB na Malaria
UNDP South Sudan/Brian Sokol

Vifo vinavyotokana na VVU, TB na Malaria vinaweza kuongezeka maradufu katika miezi 12 ijayo-Ripoti

Ripoti mpya ya  fuko la kimataifa la ufadhili Global Fund iliyotolewa leo mjini Geneva Uswisi inakadiria kuwa nchi ambazo zimeathirika na Virusi Vya UKIMWI, VVU, Kifua Kikuu yaani TB na Malaria, kwa haraka zinahitaji dola bilioni 28.5 za kimarekani ili kulinda hatua kubwa zilizokwisha kufikiwa katika miongo miwili iliyopita katika mapambano dhidi ya magonjwa hayo matatu.