Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.
Taarifa kuhusu Virusi vya Corona
Mashirikisho na jumuiya 200 yaonesha mshikamano na waathirika wa COVID-19 wanaobaguliwa
Viongozi wa jumuiya za ughaibuni na mashirika ya kijamii kutoka kote duniani wamekuja pamoja kutuma ujumbe ulio bayana na wa mshikamano na watu wanaokabiliwa na vitendo vya chuki dhidi ya wageni, ubaguzi na hata ukatili kutokana na janga la corona au COVID-19 kwa mujibu wa shirika la Umoja wa Mataifa la uhamiaji IOM.
Michoro na picha vyasaidia wakuchi kuelewa jinsi ya kujikinga na Corona
Nchini Afghanistan, hatua za kuzuia watu kuchangamana kwa lengo la kuepusha kusambaa kwa ugonjwa wa virusi vya Corona, COVID-19, zimesababisha watu wapatao milioni 1.5 nchini humo kukabiliwa na njaa na ugumu wa maisha.
Mimi kama mbunge ni wajibu wangu kuielimisha jamii jinsi ya kujikinga na COVID-19-Mbunge David Karubanga wa Uganda
Leo ni siku ya mabunge duniani ambapo mchango muhimu wa mabunge na wabunge unatambuliwa katika kuwawakilisha wananchi na kupaza sauti zao ili serikali imweke mwanajamii katika katika vipaumbele vyake inapoweka mipango ya nchi. Katika zama hizi za COVID-19, mabunge na taasisi nyingine za serikali nazo zimelazimika kwa kiasi fulani kufuata utaratibu mpya kujikinga na virusi ikiwemo kuweka umbali kati ya mtu na mtu na hata wakati mwingine kulazimika kufanya kazi nje ya majengo ya bunge kama ilivyo kawaida.
Somalia yapongezwa kwa upimaji wa COVID-19
Mwakilishi maalum wa Umoja wa Mataifa nchini Somalia James Swan ameipongeza serikali ya Somalia kwa juhudi kubwa inazozifanya katika upimaji wa virusi vya corona au COVID-19 baada ya leo kuzuru maabara ya taifa ya afya ya umma (NPHRL) mjini Moghadishu.
Huduma ya afya haipaswi kuwa biashara bali haki ya binadamu:Byanyima
Mkurugenzi mtendaji wa shirika la Umoja wa Mataifa linalopambana na ukimwi UNAIDS Winnie Byanyima amesema janga la corona au COVID-19 limeongeza adha kwa watu wanaoishi na VVU lakini pia kuyumbisha uchumi wa dunia na kuongeza pengo la usawa wa kijinsia, hivyo ameisihi dunia kuchukua hatua zinaozingatia haki za binadamu kama njia pekee ya kulidhibiti janga hilo.
UNICEF yafikisha msaada wa COVID-19 kwa nchi zaidi ya 100 licha ya changamoto
Shirika la Umoja wa mataifa la kuhudumia watoto UNICEF limesema licha ya changamoto lukuki limefanikiwa kufikisha msaada kwa nchi zaidi ya 100 kupambana na janga la corona au COVID-19 na kuokoa maisha ya mamilioni ya watu.
Katika ripoti yake iliyotolewa leo mjini New York na Copenhagen, UNICEF imesema wakati janga la COVID-19 likipindua maisha ya mamilioni ya watoto kote duniani , UNICEF inafikisha msaada wa kuokoa maisha licha ya kukabiliwa na vikwazo vingi na vikubwa ikiwemo masuala ya usafiri na matatizo ya kiufundi.
UNMISS yashirikiana na Kanisa Katoliki kusambaza barakoa katika masoko ya Yambio Sudan Kusini
Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini, UNMISS, ili kusaidia kuwakinga watu dhidi ya COVID-19, umeunganisha nguvu na Kanisa Katoliki jimbo la Yambio-Tambura kusambaza barakoa zilizotengengenezwa kienyeji kwa jamii za maeneo hayo.
Vifo vinavyotokana na VVU, TB na Malaria vinaweza kuongezeka maradufu katika miezi 12 ijayo-Ripoti
Ripoti mpya ya fuko la kimataifa la ufadhili Global Fund iliyotolewa leo mjini Geneva Uswisi inakadiria kuwa nchi ambazo zimeathirika na Virusi Vya UKIMWI, VVU, Kifua Kikuu yaani TB na Malaria, kwa haraka zinahitaji dola bilioni 28.5 za kimarekani ili kulinda hatua kubwa zilizokwisha kufikiwa katika miongo miwili iliyopita katika mapambano dhidi ya magonjwa hayo matatu.
Wakati wa COVID-19, sanaa ya kuchora yawa kimbilio la mkimbizi
Kipaji na mapenzi ya uchoraji wa sanaa vimempatia mkimbizi kutoka Eritrea anayeishi nchini Libya faraja na matumaini wakati huu wa zama za janga la ugonjwa wa virusi vya Corona, au COVID-19, linalogubikwa pia na mapigano na kudorora kwa hali ya kiuchumi na kijamii katika taifa hilo la Afrika Kaskazini.
Sanaa ya kuchora yawa kimbilio la mkimbizi wakati wa COVID-19
Kipaji na mapenzi ya uchoraji wa sanaa vimempatia mkimbizi kutoka Eritrea anayeishi nchini Libya faraja na matumaini wakati huu wa zama za janga la ugonjwa wa virusi vya Corona, au COVID-19, linalogubikwa pia na mapigano na kudorora kwa hali ya kiuchumi na kijamii katika taifa hilo la Afrika Kaskazini.