Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au coronavirus">COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.
Taarifa kuhusu Virusi vya Corona
Tumejizatiti kuepusha maambukizi ya COVID-19 - CCBRT
Nchini Tanzania hospitali ya CCBRT imechukua hatua za uhakika kuhakikisha kuwa watu wenye ulemavu, wakiwemo wafanyakazi wake wanajikinga ipasavyo dhidi ya ugonjwa wa virusi vya Corona au COVID-19.
Watumishi wa umma wapongezwa na UN kwa huduma na mchango muhimu
Wakati dunia ikiendelea kupambana na janga la corona au COVID-19 Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres leo amewaenzi watumizi wa umma walio mstari wa mbele katika kupambana na janga hili na pia kwa huduma yao ya muhimu kwa binadamu.
Sudan Kusini, Sudan, CAR, Libya na Haiti kunufaika na ufadhili wa OCHA/CERF
Taarifa iliyotolewa hii leo na ofisi ya Umoja wa Mataifa inayoshughulikia misaada ya dharura, OCHA imeeleza kuwa Mratibu Mkuu wa misaada ya dharura ya kibinadamu kwenye Umoja wa Mataifa ambaye pia ni mkuu wa, Mark Lowcock, hii leo ameachia dola za kimarekani milioni 25 kutoka mfumo mkuu wa dharura wa Umoja wa Mataifa, CERF kwenda kwa shirika la Umoja wa Mataifa la uhamiaji, IOM ili kusaidia mashirika yasiyo ya kiserikali yaliyoko mstari wa mbele katika kutoa hudua ya afya ya kuokoa maisha, huduma za maji na za kujisafi katika mapambano dhidi ya COVID-19 katika Jamhuri ya Afrika ya kati, Haiti, Libya, Sudan Kusini na Sudan.
COVID-19 imetumbukiza wajane katika hali ngumu zaidi - Guterres
Ikiwa leo ni siku ya wajane duniani Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametaka kuangaziwa zaidi kwa kundi linalosahaulika mara kwa mara, wajane, hususan wakati huu wa janga la ugonjwa wa virusi vya Corona au COVID-19.
Mr. Bean aunga mkono vita ya WHO dhidi ya COVID-19
Shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO limeweka wazi hii leo kuwa kwa kushirikiana na makampuni mawili ya utengenezaji filamu wameungana na kuzindua tangazo kwa umma lililomshirikisha mchekeshaji nyota duniani Mr Bean kwa lengo la kuwaelimisha wanajamii kuhusu kujikinga na virusi vya Corona.
Utafiti wa UNAIDS waonesha COVID-19 kuathiri upatikanaji na gharama za ARVs
Utafiti mpya uliofanywa na shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na masuala ya ukimwi UNAIDS, umeonyesha uwezekano wa athari za janga la corona au COVID-19 katika nchi za kipato cha chini na cha wastani kote duniani katika upatikanaji wa dawa za kupunguza makali ya ukimwi au ARV’s.
Mkimbizi atumia stadi za uchungaji kunusuru watu na COVID-19
Nchini Kenya katika kambi ya wakimbizi ya Kakuma, Djuba Alois mkimbizi mwenye umri wa miaka 75 kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, anatumia kipawa chake cha uhubiri kuelimisha watu kuhusu ugonjwa wa virusi vya Corona, COVID-19 na jinsi ya kujikinga.
MINUSCA yabisha hodi magerezani CAR
Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kuweka utulivu nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, MINUSCA na shirika la mpango wa maendeleo la Umoja wa Mataifa, UNDP wamepatia gereza kuu la Ngaragba msaada wa vifaa vya kusaidia kuepusha kuenea kwa ugonjwa wa virusi vya Corona au COVID-19 gerezani humo.
Usivae barakoa wakati unafanya mazoezi-WHO
Wakati ugonjwa wa virusi vya Corona au COVID-19 ukiendelea kuenea katika maeneo mbalimbali duniani huku kwingine ukiwa unadhibitiwa, shirika la afya la Umoja wa Mataifa, linaendelea kutoa madokezi kadhaa ili kuhakikisha kuwa mbinu za kujikinga dhidi ya ugonjwa huo hazigeuki na kuwa mwiba kwa mhusika.
Dexamethasone waachiwe wagonjwa mahututi wa COVID-19, kulikoni?
Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO, limekaribisha matokeo ya awali uchunguzi unaoonesha kuwa dawa ya Dexamethasone, inaweza kuokoa maisha ya wagonjwa mahututi wa Corona au COVID-19.