Kuangazia suluhisho kutabadilisha hali katika eneo hili tete la Sudan na Sudan Kusini -Filippo Grandi
Kupata suluhisho zinazotegemea amani na maendeleo ni muhimu kwa mustakabali wa watu karibu milioni saba waliolazimika kuhama kwa lazima makwao kutoka Sudan na Sudan Kusini, amesema kamishna mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR Filippo Grandi kufuatia ziara yake ya siku tatu katika mwezi huu wa Agosti kwenye nchi hizo mbili, ziara ambayo imeweka wazi kuwa watu wanaorejea kutoka ukimbizini katika nchi hizo wanarudi na kukuta nyumba zao zimeharibiwa, na miundombinu haitoshi au hakuna huduma za kijamii.