Mimba za utotoni sio kupenda kwetu – Wasichana Morogoro
Kwa mujibu wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulika na Watoto – UNICEF, ndoa za utotoni ni zile zote zinanofungwa kabla ya wanandoa kufikia umri wa miaka 18, huu ni ukiukwaji wa haki za binadamu. Japokuwa sheria zinapinga ndoa hizi, lakini tabia hii mbaya bado inaendelea ulimwenguni kote. Mbaya zaidi kuwa mara nyingi mimba hizo zinakatisha haki ya elimu kwa watoto hao kwani hushindwa kuendelea na masomo kutokana na sera na sheria za nchi zao.