Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Makala

TAHA

UNDP na TAHA nchini Tanzania wajenga vituo vitano vya kuhifadhi na kufungasha mazao

Umoja wa Mataifa unapigia chepuo mifumo sahihi ya chakula inayolenga kuongeza mnyororo wa thamani kuanzia shambani hadi kwa mlaji. Hatua hii siyo tu inasaidia kutokomeza njaa bali pia inaongeza kipato kwa mkulima na ustawi kwa mlaji kwa kuwa zao ambalo linapatikana eneo moja la dunia linaweza kusafirishwa katika ubora wake na kufikia eneo lingine la dunia katika ubora huo huo.

Sauti
7'56"
© UN-Habitat /Julius Mwelu

Tunaandaa mashindano mbalimbali ya michezo ili kuwaondoa vijana kwenye mawazo mabaya - ETCO

Mara kwa mara Umoja wa Mataifa umeendelea kusisitiza kuwa vipaji vikiwemo vya michezo vina mchango mkubwa katika kusaidia kuleta maendeleo na amani.

Vijana wanapotambuliwa vipawa vyao wanapata shughuli rasmi za kufanya na hivyo kuinua vipato vyao, kuwaondoa katika mazingira hatarishi na faida nyingine za ujumla ambazo muunganiko wake unasaidia kuelekea katika kutimiza malengo ya maendeleo endelevu, SDGs.

Sauti
3'7"
© UNFPA Myanmar/Yenny Gamming

Wazazi tulinde watoto wetu dhidi ya mimba katika umri mdogo - Catherine Kobusinge Kamanyire

Nchini Uganda ripoti kutoka wilaya mbalimbali zinaonesha ongezeko la idadi ya wasichana waopata mimba utotoni kuliko wakati wowote kabla ya shule kufungwa kutokana na COVID-19. Wakati wilaya ya Hoima pekee imeripoti mimba za utotoni zaidi ya 6,000 wilaya jirani ya Masindi imeripoti zaidi ya wasichana 1,500 waliopata mimba kati ya mwezi Januari na Juni mwaka huu.

Uganda ina takribani wilaya 135.

Sauti
3'53"
Stephan Gladieu/World Bank

Mradi wa Benki ya Dunia waleta tumaini kufikia ajenda 30, Uganda

Mradi wa kuhakikisha maendeleo endelevu katika eneo lenye rasilimali ya mafuta nchini Uganda umeleta matumaini ya kukabili umaskini baada ya masoko kujengwa na barabara kadhaa katika wilaya tatu za eneo hilo.Je, mradi huo wa ARSDP unaofadhiliwa na Benki ya Dunia unasaidiaje? Basi ungana na mwandishi wetu wa Uganda John Kibego ambaye emezungumuza na viongozi wa mitaani kwenye ziara ya ukaguzi ya waziri wa maendeleo ya miji. 

Sauti
3'26"