Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Makala

Photo FAO/Marco Salustro

Matunda ni lishe muhimu katika mlo wa kila siku

Emmanuel Mwanjisi ni Afisa lishe kutoka hospitali ya Consolatha, Ikonda, katika wilaya ya Makete, nyada za juu kusini mwa Tanzania, akieleza faida za ulaji wa mbogamboga na matunda katika mwili wa binadamu ameeleza kuwa wataalamu wa lishe wanapohamasisha ulaji wa matunda hawamaanishi kuwa ni lazima mlaji ale kiasi kikubwa cha matunda hayo bali kiasi chochote hata kipande kidogo lakini mara kwa mara, kinasaidia kuleta faida mwilini. 

Sauti
3'50"
© FAO-Magnum Photos/Alex Webb

Wengi wetu hatukamilishi makundi yote matano ya chakula-Afisa Lishe Mwanjisi.

Emmanuel Mwanjisi ni Afisa lishe kutoka hospitali ya Consolatha, Ikonda, katika wilaya ya Makete, nyada za juu kusini mwa Tanzania, anaeleza faida za ulaji wa mbogamboga na matunda katika mwili wa binadamu ikiwemo kuimarisha kinga za mwili. 

Bwana Emmanuel anaeleza kuwa baadhi ya watu wamekuwa wakila milo ambayo haizingatii makundi matano ya chakula, na mara nyingi makundi ya mbogambona na matunda ndio yanayoondolewa katika mpangilio wa vyakula na matokeo yake kutetereka kwa afya za wanadamu. 

UN Tanzania/Ahimidiwe Olotu

Tunatumia muarobaini kuzuia wadudu waharibifu wa mboga za majani- Bi. Kibasa

Katika mwaka huu wa mboga za majani na matunda, Umoja wa Mataifa kupitia shirika lake la chakula na kilimo, FAO, unataka utumike kama njia ya kuibua fursa mpya za kuendeleza lishe na kipato kupitia vyakula hivyo. Mathalani maeneo ya mijini, FAO inasema mbinu bora zinaweza kupatia fursa wakazi kulima mboga za majani na hata matunda na kuuza au hata wao kula wenyewe na kuimarisha afya na kipato. Afya huanzia shambani na hivyo matumizi ya mbolea sahihi ni jambo la msingi.

UN Tanzania/Ahimidiwe Olotu

Kilimo cha mjini ndio mwendo wa sasa- Bi. Kibasa 

Katika mwaka huu wa mboga za majani na matunda, Umoja wa Mataifa kupitia shirika lake la chakula na kilimo, FAO, unataka utumike kama njia ya kuibua fursa mpya za kuendeleza lishe na kipato kupitia vyakula hivyo. Mathalani maeneo ya mijini, FAO inasema mbinu bora zinaweza kupatia fursa wakazi kulima mboga za majani na hata matunda na kuuza au hata wao kula wenyewe na kuimarisha afya na kipato. Hivyo ndivyo imekuwa kwa Mary Kibasa na wenzake huko jijini Dar es salaam, ambako wanalima mboga eneo la Kinondoni, katikati ya wakazi huku wakizingatia afya siyo tu za kwao bali za walaji.

Sauti
4'23"
UNICEF/Giacomo Pirozzi

Wakimbizi na changamoto ya kupata matunda na mboga Uganda.

Jamii ya wakimbizi ni miongoni mwa jamii zilizo hatarini kukabiliwa na utapiamlo kutokana na kutokuwa na mazingira bora ya kushiriki kwenye kilimo hasa upanzi wa mbogamboga na matunda. Pia kutokana na hali ya utegemezi wa msaada wa kibinadamu, wengi wao huwa hawana uwezo wa kununua matunda haya au mbogamboga. Licha ya changamoto hizo, juhudi zimekuwa zikifanywa ambazo zimeleta nuru hasa kwa kuwafundisha wakimbizi kutumia mbinu bunifu kupanda mbogamboga majumbani kwao. 

Sauti
3'40"
© FAO/Manan Vatsyayana

Tulime mbogamboga na matunda, zitatufaa kwa biashara na matumizi binafsi-Makete, Tanzania

Katika mwendelezo wa mfululizo wa makala za mbogamboga na matunda, ikiwa ni sehemu ya hamasa zinazoendelea ndani ya mwaka huu wa 2021 uliotangazwa kuwa mwaka wa mbogamboga na matunda, kutoka wilaya ya Makete, mkoani Njombe Tanzania, Zawadi Kikoti wa redio washirika Green FM anazungumza na baadhi ya wananchi kuhusu uelewa wao katika ulaji wa mbogamboga na matunda. 

Sauti
3'36"
UN/ John Kibego

Tunatumia Sombe (Kisamvu) ili mama mzazi apate maziwa- Scovia 

Makala hii ni sehemu ya pili ya mahojiano kati ya mwandishi wa UN News Kiswahili nchini Uganda John Kibego wa Uganda na Scovia Atuhura Habimana, mkazi wa Uganda, mkimbizi kutoka Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, DRC. Katika sehemu ya kwanza Scovia alianza kueleza umuhimu wa aina mbalimbali za mboga za majani na matunda kwa wasichana na wanawake.

Sauti
3'38"
UN/ John Kibego

Kwetu DRC mboga za majani ni muhimu kwa mzazi- Scovia

Mboga za majani zinathaminiwa kitamaduni karibu katika jamii zote barani Afrika, huku kila jamii ikiwa na aina ya mbogamboga tofauti na jamii nyingine ingawa kiafya mboga za majani ni muhimu katika kulinda mwili wa binadamu. Licha ya umuhimu baadhi ya watu wanashindwa kupata mboga za majani iwe ni kwa sababu ya kutokuwepo au kukosa kipato cha kununua.

Sauti
3'32"
© FAO/Miguel Schincariol

Ulaji wa mbogamboga na matunda siyo suala la kipato, ni uelewa. 

Mkoa wa Njombe, ni miongoni mwa mikoa iliyoko nyanda za juu kusini mwa Tanzania. Eneo hili linatajwa kuwa lenye rutuba ambalo lina mazingira mazuri ya kuweza kustawisha mbogamboga na matunda ya aina mbalimbali kama vile matufaa, parachichi na mengine mengi. Laicha ya hali hiyo, mkoa huu ni miongoni mwa maeneo yenye watu wenye utapiamlo, ukitajwa kuwa na asilimia 53.6 ya watu wake wenye utapiamlo.  

Sauti
4'2"