Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Makala

ITU

Tanzania inajitahidi kujumuisha wanawake katika TEHAMA: Injinia Ichokeleza

Sekta ya habari na mawasiliano kwa muda mrefu hasa kwenye mataifa yanayoendelea imekuwa ikitawaliwa na wanaume. Lakini katika zama hizi za utandawazi na umuhimu wa malengo ya maendeleo endelevu, SDGs yanayohimiza yeyote asiachwe nyuma na treni ya maendeleo ya 2030. Nchi zimeanza kuchukua hatua kwa chagizo la Umoja wa Mataifa kujumuisha wanawake katika TEHAMA. Nchini Tanzania serikali imeweka mikakati ikihusisha kuhamasisha jamii wakiwemo wazazi kuwachigiza watoto wao wa kike kuingia katika masomo yahusianayo na TEHAMA.

Sauti
4'49"
Picha: IFAD/GMB Akash

Kijana na ajira nchini Tanzania

Nchini Tanzania kijana Richard Hamisi baada ya kuhitimu shahada yake ya biashara na fedha katika Chuo Kikuu Mzumbe, mwaka jana wa 2018, ameandika wazo la kuanzisha maghala ya kutunzia nafaka katika maeneo yanayozalisha mazao mengi nchini huko kama njia mojawapo ya kuhakikisha mazao yanatunzwa vyema na hivyo uhakika wa chakula na bei nzuri  ya mazao. Akihojiwa na Flora Nducha wa Idhaa ya Kiswahili  ya Umoja wa Mataifa jijini Dar es Salaam, Richard amefafanua kuhusu maghala hayo na kwanza anaanza kwa kueleza alivyopata wazo la kuanzisha mradi huu.

Sauti
2'9"
UN News/Nam Cho

Mada kwa kina- Biashara mtandao

Ijumaa ya leo mada kwa kina inamulika biashara  mtandao na manufaa yake kwa jamii hivi sasa hususan zile ambazo wakazi wake wanatumia simu za mkononi na wana uwezo wa kupata mtandao wa intaneti unaowaunganisha kwenye mitandao ya kijamii kama vile Facebook, Instagram na Twitter. Grace Kaneiya amefuatilia kwa kina hali ilivyo Afrika Mashariki hususan Kenya, Tanzania na Uganda na wapigaji chepuo mada hii UNCTAD ambayo ni kamati ya biashara na  maendeleo ya Umoja  wa Mataifa. Karibu!

Sauti
7'39"
FAO/Claudia Nicolai

CIAT na utafiti wa maharage nchini Uganda

Katika kurejelea baadhi ya habari zilizokuwa na mvuto zaidi mwaka uliopita wa 2018, tunarejea nchini Uganda hususan kwenye kituo cha kimataifa cha utafiti wa kilimo kwa nchi za kitropoki, CIAT ambako tulizungumza na Robin Buruchara, mtafiti wa maharagwe katika kituo hicho.

Sauti
4'10"
Picha: UNICEF/Al-Zikri

Elimu ya ufundi, suluhisho la ukosefu wa ajira nchini Uganda.

Ukosefu wa ajira bado ni moja ya changamoto kubwa ulimwenguni kote hususan miongoni mwa vijana wanaohitimu masomo ambayo kwa kiasi kikubwa yamewaelekeza katika kazi za kuajiriwa. Nchini Uganda takwimu zinazoonesha kuwa asilimia 80 ya wahitimu hawana ajira, imeisukuma serikali ya nchi hiyo kuanzisha kampeni ya kuhamasisha vijana kujiunga na elimu ya kuwawezesha kupata stadi za ufundi.

Sauti
3'40"