Kijana na ajira nchini Tanzania
Pakua
Nchini Tanzania kijana Richard Hamisi baada ya kuhitimu shahada yake ya biashara na fedha katika Chuo Kikuu Mzumbe, mwaka jana wa 2018, ameandika wazo la kuanzisha maghala ya kutunzia nafaka katika maeneo yanayozalisha mazao mengi nchini huko kama njia mojawapo ya kuhakikisha mazao yanatunzwa vyema na hivyo uhakika wa chakula na bei nzuri ya mazao. Akihojiwa na Flora Nducha wa Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa jijini Dar es Salaam, Richard amefafanua kuhusu maghala hayo na kwanza anaanza kwa kueleza alivyopata wazo la kuanzisha mradi huu.
Audio Credit
Grace Kaneiya/ Flora Nducha /Richard Hamisi
Sauti
2'9"