08 DESEMBA 2023
Hii leo kwenye jarida Assumpta Massoi anamulika mzozo Mashariki ya Kati hususan huko Gaza, nyaya za simu zageuzwa kuni, kisha anakwenda Mashariki mwa Afrika huko baada ya ukame wa muda mrefu sasa ni mvua za kupindukia zinazosababisha maafa makubwa,; makala anakupeleka Tanzania kusikia uchambuzi wa Ibara ya 15 ya Tamko la Haki za Binadamu la UN, na mashinani utamsikia binti shujaa wa mazingira kutoka visiwani Zanzibar nchini Tanzania.