Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari kwa Ujumla

UNICEF Kenya/2023/Translieu

Mradi wa "Njoo shuleni" nchini Kenya warejesha matumaini kwa familia

Elimu ni moja ya nyenzo zenye nguvu zaidi za kuleta mabadiliko kwa watu binafsi na jamii na ndio maana katika miongo miwili iliyopita, serikali ya Kenya imefanya mageuzi mengi ili elimu ya msingi iwe bure na ya lazima kwa watoto wote walio katika umri wa kwenda shule. 

Hata hivyo, watoto wengi bado hawako shuleni kutokana na umaskini, miundombinu duni, kutelekezwa na wazazi na matatizo ya kiafya hasa katika maeneo masikini. Sasa shirika la Umoja la kuhudumia watoto UNICEF limeamua kuingilia kati kwa kushirikiana na wadau kusaidia. Flora Nducha na maelezo zaidi.

Sauti
2'53"
© UNHCR/Insa Wawa Diatta

Hali si swari Burkina Faso msirejeshe wakimbizi wake: UNHCR

Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi UNHCR, leo limetoa mwongozo mpya juu ya ulinzi wa watu wanaokimbia Burkina Faso, na wito wa haraka kwa mataifa yote kuacha kuwarudisha kwa nguvu watu wote wanaotoka katika ukanda huo ulioathiriwa zaidi na mgogoro unaoendelea nchini humo na badala yake kuwaruhusu raia wanaokimbia Burkina Faso kuingia katika mipaka yao. 

Sauti
2'33"

28 JULAI 2023

Hii leo jaridani tunaangazia afya na hali ya usalama na msaada wa kibinadamu nchini Burkina Faso. Makala tnamulika harakati za kufanikisha SDGs na mashinani tunakupeleka nchini Kenya, kulikoni? 

Sauti
10'54"
UNICEF/Ilvy Njiokiktjien

Dkt. Tedros - Tunaishi mara moja na tuna ini moja, tutokomeze Homa ya Ini

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Ulimwenguni (WHO) Dkt. Tedros Adhanom Ghebreyesus kupitia ujumbe wake kwa Siku ya Kimataifa ya Homa ya Ini inayoadhimishwa kila Julai 28, amesema kwa kuwa wanadamu tunaishi mara moja na tuna ini moja, WHO imejitolea kushirikiana na nchi zote na wadau wote ili kutimiza maono ya pamoja ya kutokomeza virusi vya homa ya ini ifikapo 2030.  

Sauti
1'59"
UNFPA Video

Hospitali Sudan zaomba usaidizi

Vita nchini Sudan ambayo sasa imedumu kwa zaidi ya siku 100 imeshuhudia zaidi ya watu milioni 3 wakiyakimbaia makazi yao kwenda kusaka hifadhi katika miji mingine pamoja na nchi Jirani. 

Video ya shirika la Umoja wa Mataifa la idadi ya watu na afya ya uzazi UNFPA inaanza kwa kuonesha chupa cha upasuaji ambako mjamzito amefanyiwa upasuaji na kujifungua salama huko katika mji Port Sudan jimboni Red Sea mashariki mwa nchi ya Sudan.

Sauti
2'41"
© UNICEF/Frank Dejongh

UNESCO inasema teknolojia itumike kwa manufaa ya mwanadamu na sio kuwa mbadala wake: Ripoti

Ripoti mpya iliyotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la elimu , sayansi na utamaduni UNESCO kuhusu ufuatiliaji wa teknolojia katika elimu GEM 2023 imetaka mifumo ya elimu kote duniani siku zote kuhakikisha kwamba matakwa ya wanaojifunza yanakuwa katika kitovu cha teknolojia na kwamba teknolojia zitumike kusaidia elimu inayotokana na mwingiliano wa binadamu badala ya kulenga kuwa mbadala wake. 

Ripoti hiyo mwaka 2023 ya GEM inashughulikia matumizi ya teknolojia katika elimu duniani kote kupitia muktadha wa umuhimu, usawa, uthabiti na uendelevu.

Sauti
3'6"
© WFP/Michael Tewelde

Guterres ataja mambo matatu ya kufanikisha mifumo bora ya chakula duniani

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres amezungumza kwenye mkutano wa viongozi kuhusu Mifumo ya Upatikanaji wa Chakula huko Roma, Italia hii leo akisema bado inastaajabisha kuwa katika dunia yenye utajiri bado kuna watu hawana chakula au wanakufa njaa, huku akipendekeza mambo makuu matatu ya kuzingatia ili kurekebisha mifumo hiyo. Assumpta Massoi na maelezo zaidi

Sauti
2'20"
WHO/PAHO/Luz Sosa

WHO: Nusu ya watu duniani hatarini kuugua Dengue

Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ulimwenguni WHO limesema takriban nusu ya idadi ya watu ulimwenguni hivi sasa wapo hatarini kuungua ugonjwa wa Dengue huku ikikadiriwa kila mwaka watu kati ya milioni 100 mpaka 400 wanapata maambukizi. 

Dengue ni ugonjwa unaoenezwa na mbu aina ya Aedes. Ugonjwa huo hutokea zaidi katika nchi zenye hali ya hewa ya kitropiki na ya joto. 

Sauti
2'35"