Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari kwa Ujumla

TANBAT 6/Kapteni Inyoma

Walinda amani kutoka Tanzania watoa mafunzo ya mapishi na ujasiriamali kwa wanawake wanakijiji cha Moro, CAR

Walinda amani wa Umoja wa Mataifa wa kikosi cha 6 kutoka Tanzania (TANBAT 6) wanaohudumu chini ya Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Afrika ya kati, CAR (MINUSCA) wametoa mafunzo ya upishi kwa vikundi vya wanawake wa Kijiji cha Moro kilichoko takribani kilometa 50 kutoka Mji wa Berberati, jimboni Mambere Kadei yalipo makao makuu ya kikosi hicho.  

Sauti
2'11"
UNODC

Usambazaji wa Dawa za Kulevya umezidisha mizozo ya kimataifa, ripoti ya UNODC yaonya

Kuendelea kwa ongezeko la usambazaji haramu wa dawa za kulevya na mitandao ya usambazaji inayoendelea kukua inazidisha mizozo ya kimataifa na changamoto za huduma za afya na utekelezaji wa sheria, imesema Ripoti ya Dunia ya Dawa za kulevya mwaka huu 2023 iliyozinduliwa leo na Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kupambana na Dawa za Kulevya na Uhalifu (UNODC). 

Sauti
3'23"
UN/ Stella Vuzo

UNESCO inaungana na Afrika kuenzi Kiswahili - Estelle Zadra

Maadhimisho ya pili ya siku ya lugha ya Kiswahili duniani yatafanyika wiki ijayo Julai 7 na sasa maandali zi yanafanyika katika kila kona kuhakikisha siku hiyo iliyopewa uzito mkubwa na shirika la Umoja wa Mataifa la elimu , sayansi na utamaduni UNESCO lakini pia inatumika kama jukwaa la kuziunganisha jamii sio za Afrika tu zinazozungumza Kiswahili ali na nyinginezo zinazokumbatia Kiswahili.

Sauti
3'25"
© UNOCHA/Laurent Dufour

Watumishi wa umma wanachangia ujenzi wa mustakbali bora kwa wote: Guterres

Leo ni siku ya Umoja wa Mataifa ya watumishi wa umma, ambapo katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amesema mchango wao ni muhimu sana katika ufanikishaji wa malengo ya maendeleo endelevu na kuhakikisha mustakbali bora kwa wote.

Antonio Guterres katika ujumbe wake wa siku hii amesema lengo lake ni kuwaenzi wanawake na wanaume kote duniani ambao huwajibika kwa jukumu muhimu zaidi la kutoa huduma kwa umaa.

Sauti
1'42"
© UNICEF/Aleksey Filippov

Umoja wa Mataifa imelaani vikali shambulio lililoua na kujeruhi wafanyakazi wa ukoaji Kherson Ukraine

Mratibu wa masuala ya kibinadamu wa Umoja wa Mataifa nchini Ukraine Matthew Hollingworth amelaani vikali shambulio lililofanywa na Urusi kwenye eneo la Kherson lililoathirika vibaya na mafuriko ya bwawa la Kakhovka, na kukatili maisha ya mfanyakazi wa ukoaji na kujeruhi wengine. 

Katika tarifa yake iliyotolewa leo mjini Kyiv  Ukraine mratibu huyo Hollingworth amesema “Inasikitisha sana kwamba waokoaji wameuawa na kujeruhiwa jana huko Kherson walipokuwa wakisaidia jamii zilizoathiriwa na uharibifu mkubwa wa bwawa la Kakhovka.”

Sauti
1'39"
© UNHCR/Pauline Omagwa

Wakimbizi Kenya: Mradi wa shiriki ni neema kwetu na jamii inayotuhifadhi

Serikali ya Kenya inaendesha mradi wa “shiriki” ambao unawapa fursa wakimbizi wanaosihi katika kambi ya wakimbizi ya Kakuma iliyoko katika kaunti ya Turkana nchini humo kujitegemea kwa kufanya kilimo cha mbogamboga kupitia chama cha ushirika wa wakulima. Serikali hiyo imetenga ekari 21katika kambi ya Kakuma ili kutumika katika mradi huo ambao sio tu unawapa lishe bora wakimbizi, matumaini na kipato lakini pia umekuwa neema kwa jamii za wenyeji.

Sauti
3'17"
Screen capture

Kina mama wa Srebenica waeleza athari za kauli za chuki

Hapo jana juni 18 dunia iliadhimisha siku ya kimataifa ya kupinga kauli za chuki ambapo katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York Marekani kumefanyika maonesha ya athari ziletwazo na kauli za chuki. Wawakilishi watatu wa taasisi ya Kina mama wa Srebrenica walitembelea maonesho hayo na kuzungumzia maswahibu yaliyowakumba miaka 28 iliyopita na kuacha vidonda katika mioyo yao. 

 

Taarifa ya Leah Mushi

Sauti
3'57"
Picha: FAO/Albert González Farran

Jamii ya Wavuvi Sudan Kusini wawezeshwa na FAO kutengeneza mnyororo wa thamani

Mkuu wa Mpango wa umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Sudan Kusini UNMISS ambaye pia ni mwakilishi wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini humo Nicholas Haysom amefanya ziara maalum ya kutembelea visiwa vilivyopo katika kaunti ya Terekeka na kujionea utekelezaji wa miradi ya stadi za maisha inayoendeshwa na shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo FAO. 

Sauti
3'3"