Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari kwa Ujumla

UN News/ Byobe Malenga.

Mada kwa kina: Chanjo dhidi ya Kipindupindu yaendelea Kivu Kaskazini, DRC

Kampeni ya utoaji wa chanjo dhidi ya ugonjwa wa kipindupindu  iliyoanza tarehe 25 mwezi huu huko Kivu Kaskazini nchini jamhuri ya Kidemokraia ya Congo, DRC imekunja jamvi jana Jumanne ya tarehe 30 mwezi hu uwa Januari ambapo shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni WHO lilizindua kampeni hiyo ya chanjo kwa wakimbizi wa ndani katika kambi ya wakimbizi hao ya Kanyaruchinya wilayani nyiragongo katika mji wa Goma jimboni Kivu Kaskazini.

Sauti
5'30"
UNHCR Video

Jamii ya Benet nchini Uganda yaiomba utaifa: UNHCR

Baada ya zaidi ya takriban miongo minane ya kutokuwa na utaifa, jamii ya watu wa asili ya Benet nchini Uganda inahaha kuishi, na kwa mujibu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR bila kuwa na nyaraka rasmi muhimu jamii hiyo haiwezi kupata huduma za msingi kama elimu na afya , na sasa jamii hiyo inaiomba serikali ya Uganda kumaliza zahma hiyo iliyowaghubika kwa miongo.

Sauti
3'6"
© UNICEF/Olivier Asselin

WHO limesema magonjwa ya kitropiki yaliyosahaulika mbioni kutokomezwa duniani

Shirika la Umoja wa MAtaifa la afya ulimwenguni, WHO, limesema mataifa mengi zaidi duniani yametokomeza magonywa ya kitropiki yaliyosahaulika, au NTDs huku ikisema bado uwekezaji zaidi unahitajika kusongesha maendeleo hayo dhidi ya magonjwa hayo kama vile ukoma, vikope na kung’atwa na nyoka.

Kauli hiyo ya WHO imetolewa leo ikiwa ni siku ya kimataifa ya kuhamasisha dhidi ya magonjwa hayo ya kitropiki yaliyosahaulika, NTDs na shirika limeweka hayo bayana kwenye ripoti mpya iitwayo Ripoti ya Dunia kuhusu NTDs kwa mwaka 2023.

 

Sauti
2'3"
TANZBATT 9

TANZBATT 9 wafanya doria barabara inayounganisha DRC na Uganda

Kufuatia mashambulizi yanayofanywa na makundi mbalimbali ya waasi kwa raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC hususani mashariki mwa nchi hiyo ya pili kwa ukubwa wa eneo barani Afrika, walinda amani wa Umoja wa Mataifa wa kikosi cha 9 kutoka Tanzania, TANZBATT 9 kinachohudumu katika kikosi cha Umoja wa Mataifa cha kujibu mashambulizi cha FIB-MONUSCO, wamefanya doria katika barabara ya Mbau-Kamango nje ya mji wa Beni jimboni Kivu Kaskazini. 

Sauti
1'45"
UN News Video/Thelma Mwadzaya

Kenya: Mradi wa Teen Seed Africa warejesha matumaini ya elimu kwa wasichana waliopata mimba za utotoni

Umoja wa mataifa kwa ushirikiano na serikali ya Kenya ulizindua mwaka 2015 mradi wa kuwarejesha watoto shule walioacha kwa sababu moja au nyengine. 

Kupitia mashirika mbalimbali kama Educate A Child, Shirika la umoja wa mataifa la kuhudumia watoto UNICEF na lile la idadi ya watu duniani UNFPA ilizindua miradi ya pamoja ya kuwarejesha watoto shule. 

Utafiti wa hivi karibuni  wa mashirika hayo umebainisha kuwa moja ya chanzo kikuu cha watoto wa kike kuacha shule ni mimba za utotoni na hususan watoto ambao wanaishi katika mitaa ya mabanda.  

Sauti
6'41"
UNOCHA

Usalama unawezarejeshwa katika sehemu za kanda ya Ziwa Chad - Niamey

Mkutano wa 3 wa Ngazi ya Juu kuhusu Kanda ya Ziwa Chad umehitimishwa leo kwa kuthibitishwa ahadi kutoka kwa nchi za Bonde la Ziwa Chad na wadau kwa mwitikio ulioratibiwa, wa kikanda na ulio endelevu.

Mkutano huo uliohitimishwa leo katika mji mkuu wa Niger, Neamey, ulilenga kuhakikisha usaidizi wa kibinadamu na ulinzi na kukuza fursa za ufumbuzi wa kudumu, ikiwa ni pamoja na kurejea, kuunganishwa tena katika jamii na kuwapa makazi wakimbizi wa ndani na wakimbizi kutoka nje kwa kuzingatia uamuzi wa wa hiari, wenye heshima na ufahamu kuhusu uamuzi huo.  

Sauti
1'55"
© UNICEF/Safidy Andriananten

WFP na serikali ya Madagascar zaungana mikono kubadilisha jamii za vijijini kusini mwa Madagascar kupitia mradi wa RTT

kupitia mradi wa mabadiliko ya haraka vijijini (RRT) shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani WFP na wadau wake wameanzisha kituo maalum cha paneli za sola ambacho ni chanzo kikuu na endelevu cha maji na teknolojia ya mawasiliano ICT katika maeneo ya vijijini nchini Madagascar, hatua inayoruhusu upatikanaji wa huduma muhimu kama vile nishati, maji na mitandao ya kijamii kwa wakazi wa jamii hizo na kwa njia inayojali mazingira.

Sauti
2'35"
Unsplash/Markus Winkler

Mabillioni ya watu ulimwenguni hawajalindwa kutokana na viambato vinavyosababisha ugonjwa wa moyo

Ripoti mpya ya Shirika la Umoja wa Mataifa la la Afya Duniani (WHO) iliyotolewa leo Jumatatu Januari 23, 2023 imebainisha kuwa watu bilioni tano duniani hawajalindwa dhidi ya viambato hatari vya mafuta vilivyoko katika bidhaa za vyakula vinazozalishwa viwandani na hivyo kuongeza hatari ya kupata magonjwa ya moyo na kifo.

Sauti
2'55"