Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari kwa Ujumla

© UNICEF/Donaig Le Du

Mashirika yashirikiana kusambaza chakula Sudan

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR nchini Sudan limesema linaendelea kufanya kazi kwa karibu na shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani, WFP ili kuona ni kwa vipi chakula kilichomo nchini humo kinawza kusambazwa kwa wahitaji na wakati huo huo misaada mingine inaweza kutolewa kwa ushirikiano na wadau wengine wakati huu ambapo uhasama unashamiri na kuathiri raia wakiwemo wakimbizi, wakimbizi wa ndani na raia nchini kote.

Sauti
2'19"
©WTO

FAO, UNWTO: Utalii milimani unaweza kuimarisha baiyonuai na vipato vya wakazi wa maeneo hayo

Ripoti mpya iliyotolewa leo na mashirika ya Umoja wa Mataifa na wadau imeeleza bayana jinsi utalii kwenye maeneo ya milimani unaweza kuwa na manufaa sio tu kwa baiyonuwai bali pia kwa jamii zinazoishi kwenye maeneo hayo.

Taarifa iliyotolewa na shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo, FAO mjini Roma, Italia hii leo imesema chapisho hilo limetolewa ili kwenda sambamba na hitimisho la mwaka wa kimataifa wa maendeleo endelevu ya milima ulioanza mwaka jana wa 2022. 

Sauti
2'11"
© UNICEF/Mojtba Moawia Moawi

UNICEF: Sudan sitisheni mzozo hali ya watoto inazidi kuwa mbaya

Msikilizaji, Usemi ambao umekuwa ukielezwa mara zote watu wanapozungumzia suala la amani ni kwamba, vita inapotokea wanaotesema ni wanawake na watoto. Kwa zaidi ya wiki moja nchi ya Sudan imekuwa katika vita ya madaraka baina ya majeshi ya nchi hiyo. Je hali ya watoto ipoje?

Hata kabla ya kuanza kwa mzozo wa hivi karibuni nchini Sudan, mahitaji ya kibinadamu kwa watoto yalikuwa juu sana. Takwimu zikionesha robo tatu ya watoto walikadiriwa kuishi katika umaskini uliokithiri, na watoto milioni 11.5 na wanajamii walihitaji huduma za dharura za maji na usafi wa mazingira.

Sauti
2'54"
© UNICEF/Kalungi Kabuye

Wakati wa COVID-19 watoto milioni 25 walikosa chanjo, ni wakati wa kuziba pengo hilo: WHO

Wiki ya chanjo ya shirika la Umoja wa Mataifa la afya duniani WHO, inaanza leo ikichagiza juhudi kubwa kufanyika ili kuziba pengo la chanjo duniani kote.

Wiki hiyo itakayo kamilika Aprili 30 huadhinmishwa kila wiki ya mwisho ya mwezi Aprili lengo likiwa ni kuainisha juhudi za pamoja zinazohitajika ili kuwalinda watu dhidi ya magonjwa yanayozuilika kwa chanjo.

Sauti
2'34"
World Bank video

Upandaji wa miti ya migunga yarejesha matumaini kwa wakazi wa msitu wa Congo

Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, mradi unaofadhiliwa na Benki ya Dunia wa kupanda miti aina ya migunga umeondoa tishio la ukataji miti holela kwenye msitu.

wa bonde la mto Congo, ambao ni wa pili kwa ukubwa duniani katika kufyonza hewa ya ukaa na sasa wananchi wananufaika sio tu kwa kupata mkaa bali pia hata watu wa jamii ya asili wanaweza kupata kitoweo porini.

Sauti
2'16"
© UNEP

Guterres: Tumieni elimu za watu wa asili kutatua changamoto za ulimwengu

Hii leo katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York Marekani Jukwaa la kudumu la watu wa asili limeanza rasmi ambapo katika ufunguzi wa jukwaa hilo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema pamoja na majukumu muhimu ya jamii za asili hususan katika kulinda mazingira na mbinu nyingine mbadala za maisha, watu hawa wanazidi kuwa masikini na kuzitaka nchi zote duniani zihakikishe zinawasaidia kuondokana na umasikini

Sauti
2'55"
UNICEF/Karel Prinsloo

Wanafunzi nchini Nigeria wahitaji ulinzi zaidi: UNICEF

Ikiwa ni miaka tisa imepita tangu wasichana 276 kutekwa nyara wakiwa katika shule ya bweni huko Chibok Nigeria ambapo mpaka sasa 96 bado wapo utumwani, Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF limetaka wadau kusaidia katika kuwekeza zaidi katika usalama wa wanafunzi mashuleni kwani bado vitendo vya utekaji vinaendelea nchini humo.

Sauti
2'14"