Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Goma waenzi walinda amani wa Tanzania, familia zalilia wapendwa wao

Mkuu wa operesheni za ulinzi wa amani za Umoja wa Mataifa Jean-Pierre Lacroix akimjulia hali mmoja wa walinda amani wa Tanzania waliolazwa kwenye hospitali mjini Goma, jimbo la Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC baada ya shambulio dhidi ya kambi yao alhamisi ya wiki iliyopita. (Picha:MONUSCO)

Goma waenzi walinda amani wa Tanzania, familia zalilia wapendwa wao

Huko Goma hii leo kwenye jimbo la Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini humo MONUSCO kunafanyika tukio maalum la kuenzi walinda amani 14 wa Tanzania waliouawa katika shambulio wiki iliyopita huku familia za walinda amani hao zikizungumzia mustakhbali wao.

Shughuli hiyo inaongozwa na mkuu wa operesheni za ulinzi wa amani za Umoja wa Mataifa Jean-Pierre Lacroix pamoja na Balozi wa Tanzania nchini DRC Ignace Meela.

Kabla ya kushiriki tukio hilo, Bwana Lacroix aliwajulia hali walinda amani wengine ambao bado wamelazwa kwenye hospitali mjini Goma na kusema...

(Sauti ya Jean-Pierre Lacroix)

“Nimeshiriki katika tukio la kutoa shukrani huko Dar es salaam na leo niko hapa. Nimetoka pia katika tukio lililoandalwa hapa Goma na pia Kampala. Hapa Goma nimetembelea askari wa Tanzania ambaao walijeruhiwa. Nimetakia ahueni ya haraka. Na nimeridhika kuwa wanahudumiwa vizuri na inatia faraja.”

image
Walinda amani wa Tanzania waliojeruhiwa kwenye shambulio la tarehe 7 mwezi disemba mwaka huu huko Semuliki, jimbo la Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC wakiwa kwenye hospitali mjini Goma wakiendelea na matibabu. (Picha:MONUSCO)
Nako nchini Tanzania wakati maziko ya walinda amani yakifanyika, baadhi ya wanafamilia wamezungumzia mustakhbali wa familia akiwemo Mohammed Khatib ambaye ni mjomba wa mlinda amani Shazil Nandonde.

(Sauti ya Mohammed Khatib)

image
Walinda amani huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC wakati wa tukio la kumbukizi ya wenzao waliouawa wiki iliyopita. (Picha:MONUSCO)
Kwa upande wake Mathilda Wakusola ambaye ni dada wa marehemu Samuel Chenga amesema.

(Sauti ya Mathilda Wakusola)

Haji Hassan Hamis kutoka Zanzibar akamzungumzia marehemu Hassan Abdallah Makame ambaye ni mtoto wa dada yake na aliwahi kuhudumu Darfur nchini Sudan na baadaye DRC ambako mauti yalimkuta.

(Sauti ya Haji Hassan Hamis)