Skip to main content

Chuja:

Semuliki

Wadau lazima watimize wajibu wao kurejesha amani DRC: Lacroix

Ili amani ya kweli na ya kudumu iweze kurejea nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, ni lazima wadau wote wa kisiasa ikiwemo serikali, chama tawala, wapinzani, asasi za kiraia na tume ya uchaguzi watimize wajibu wao katika kuhakikisha maandalizi ya uchaguzi mkuu yanaendelea kwa wakati kama ilivyopangwa.

Wito huo umetolewa na mkuu wa operesheni za ulinzi wa amani za Umoja wa Mataifa Jean-Pierre Lacroix alipotoa taarifa hii leo kwenye baraza la usalama  kuhusu hali nchini DRC na kusisitiza kuwa

(JEAN-PIERRE LACROIX-CUT 1)

Guterres kuzungumza na Rais Magufuli wa Tanzania

Kufuatia mauaji ya walinda amani 14 wa Tanzania huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC siku ya Alhamisi na wengine zaidi ya 44 kujeruhiwa, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres muda wowote sasa atazungumza kwa njia ya simu na Rais John Magufuli wa Tanzania.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki nchini Tanzania, Balozi Augustine Mahiga amesema hayo akihojiwa na Idhaa hii kwa njia ya simu kutoka Dar es salaam.

(Sauti ya Balozi Augustine Mahiga)