Wanahabari tukikatishwa tamaa tunawaangusha wananchi – Waandishi wa habari DRC
Hii leo ikiwa ni siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari duniani maudhui yakiwa Kuumba mustakabali wa Haki: Uhuru wa kujieleza kama kichocheo cha haki zote za binadamu, huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC mapigano ya mara kwa mara yamekwamisha harakati za waandishi wa habari kupatia wananchi haki yao ya msingi ya kupata habari.