Skip to main content

Chuja:

Beni

Regine Ngamanene Okando (kushoto), mwandishi wa habari wa Radio Canal Rafiki kwenye mji wa Beni jimboni Kivu Kaskazini na Erickson Luhembwe, mwandishi wa habari wa RFI katika majimbo ya Ituri na Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC…
UN News/George Musubao

Wanahabari tukikatishwa tamaa tunawaangusha wananchi – Waandishi wa habari DRC

Hii leo ikiwa ni siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari duniani maudhui yakiwa Kuumba mustakabali wa Haki: Uhuru wa kujieleza kama kichocheo cha haki zote za binadamu, huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC mapigano ya mara kwa mara yamekwamisha harakati za waandishi wa habari kupatia wananchi haki yao ya msingi ya kupata habari.

Sauti
6'28"
Mtoto akipatiwa tiba dhidi ya malaria kwenye kituo cha afya cha Gracia kwenye mji wa Beni jimboni Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC.
UN News/George Musubao

Malaria na changamoto kwa wakazi wa Beni, DRC

Hii leo ikiwa ni siku ya Malaria duniani, huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, jinamizi la Malaria bado linatikisa taifa hilo ambapo shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni , WHO, Kanda ya Afrika linasema, asilimia 96 ya wagonjwa wa Malaria duniani kwa mwaka 2022 walikuwa katika nchi 29 ikiwemo DRC.

UN/Michael Ali

Kambi ya Kamango huko Beni, DRC yafungwa na MONUSCO

Kambi ya Kamango iliyokuwa inamilikiwa na kikosi cha ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, MONUSCO imefungwa baada ya kukamilisha jukumu lake.

Kambi hiyo iliyoko kilometa 80 kaskazini-magharibi mwa mji wa Beni jimbo la Kivu Kaskazini ilianzishwa miaka 10 iliyopita kukabili vitisho kutoka waasi wa ADF na imefungwa rasmi tarehe 6 mwezi huu. 

Sauti
2'4"
Mkazi huyu wa Beni, jimboni Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC aitwaye Joel Methya Ndeku alipoteza ndugu zake katika mauaji ya mwaka 2018 na hadi leo hafahamu chochote kuhusu wauaji.
UN News/George Musubao

UN itusaidie tupate ukweli na haki kwa kuuawa kwa ndugu zetu – Mkazi Beni, DRC

Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC mashambulizi yanayoendelea mashariki mwa nchi hiyo kwenye jimbo la Kivu Kaskazini yanasababisha sio tu vifo bali machungu yasiyoisha kwa familia za waliouawa kwa kushindwa kufahamu ukweli wa nini kiliwafika jamaa zao, nani aliwaua, na haki gani imetendeka na sheria dhidi ya waliohusika. 

Sauti
4'16"
TANZBATT 9

TANZBATT 9 wafanya doria barabara inayounganisha DRC na Uganda

Kufuatia mashambulizi yanayofanywa na makundi mbalimbali ya waasi kwa raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC hususani mashariki mwa nchi hiyo ya pili kwa ukubwa wa eneo barani Afrika, walinda amani wa Umoja wa Mataifa wa kikosi cha 9 kutoka Tanzania, TANZBATT 9 kinachohudumu katika kikosi cha Umoja wa Mataifa cha kujibu mashambulizi cha FIB-MONUSCO, wamefanya doria katika barabara ya Mbau-Kamango nje ya mji wa Beni jimboni Kivu Kaskazini. 

Sauti
1'45"
Walinda amani wa Umoja wa Mataifa, Kikosi cha 9 kutoka Tanzania, TANZBATT 9 katika doria ya barabara ya Mbau-Kamango
TANZBATT 9

Walinda amani wa UN kutoka Tanzania wafanya doria barabara inayounganisha DRC na Uganda

Kufuatia mashambulizi yanayofanywa na makundi mbalimbali ya waasi kwa raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC hususani mashariki mwa nchi hiyo ya pili kwa ukubwa wa eneo barani Afrika, walinda amani wa Umoja wa Mataifa wa kikosi cha 9 kutoka Tanzania, TANZBATT 9 kinachohudumu katika kikosi cha Umoja wa Mataifa cha kujibu mashambulizi cha FIB-MONUSCO, wamefanya doria katika barabara ya Mbau-Kamango nje ya mji wa Beni jimboni Kivu Kaskazini. 

Sauti
1'45"
Wapiganaji wa M23 wakielekea Goma nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC
MONUSCO/Sylvain Liechti

Raia 18 wamejeruhiwa na 4 mahutusi katika machafuko Kivu Kaskazini DRC:UN

Taarifa kutoka mpango wa Umoja wa Mastaifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC zinasema hali katika Mashariki mwa nchi hiyo bado ni ya wasiwasi mkubwa , huku kukiwa na ripoti za mapigano kati ya wanajeshi wa serikali FRDC na kundi la wapiganaji la M23 kusini na kusini-mashariki mwa eneo la Kitchanga, katika jimbo la Kivu Kaskazini. 

TANZBATT 9 / Private Sosper Msafiri

TANZBATT 9 nchini DRC wahitimisha kampeni ya Amani na Afya kwa kukabidhi jengo

Kikosi cha 9 cha walinda amani wa Umoja wa Mataifa kutoka Tanzania wanaohudumu nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC kupitia Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo - MONUSCO wamehitimisha kampeni yao ya Afya na Amani iliyoanza tarehe 3 mwezi huu wa January ambapo  wamekabidhi jengo kwa ajili ya mahali pa wagonjwa na wahudumu wa afya kula chakula katika Kituo cha Afya cha Mavivi, mjini Beni, Jimboni Kivu Kaskazini mashariki mwa DRC.

Sauti
3'55"
Picha: MONUSCO

Walinda amani wa UN kutoka Tanzania wafikisha misaada Hospitali ya Oicha, DRC

Kikosi cha 9, TANZBATT 9 cha wanajeshi walinda amani wa Umoja wa Mataifa kutoka Tanzania wanaohudumu nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC chini ya Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo DRC-MONUSCO, wameendelea na kampeni yao ya Afya na Amani ambapo hadi tarehe 13 mwezi huu wa Januari watakuwa wakiendelea kutoa misaada kwa jamii inayoishi katika eneo lao la kazi, kaskazini mashariki mwa nchi.

Walianza na Kituo cha afya cha Mavivi na sasa ilikuwa zamu ya Hospitali ya Oicha katika mji wa Beni jimboni Kivu Kaskazini.

Sauti
2'13"