Tanzania imepiga hatua katika kuhakikisha kila mtoto anaandikishwa shuleni japo changamoto zipo
Stella Vuzo wa UNIC Dar es Salaam anamuhoji Ayubu Kafyulilo mtaalamu katika shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF nchini Tanzania anayesimamia masuala ya ujifunzaji na elimu kwa ajili ya vijana na watoto ambao wako katika mazingira magumu na walio nje ya shule. Kwanza anaanza kwa kueleza hali ya elimu ikoje nchini humo baada ya kuanza kwa mfumo wa elimu bila malipo kwa ngazi ya kuanzia elimu ya awali, msingi hadi kidato cha nne.