Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Taarifa kuhusu Virusi vya Corona

Virusi vya Corona kama dharura ya afya ya umma:Taarifa za UN News Kiswahili
Mlipuko uliripotiwa mara ya kwanza Wuhan China Desemba 31, 2019

Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au coronavirus">COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake  na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.

Dorica Zuze na mwanae akiwa katika kituo cha afya  nchini Malawi.
© UNFPA/Joseph Scott

Tusijidanganye, wimbi la tatu la Covid-19 Afrika halijaisha kabisa - WHO

Baada ya wiki nane mfululizo za kuongezeka kwa kasi ya maambukizi, sasa maambukizi mapya ya  Covid-19 barani Afrika yamepungua kasi, Afrika Kusini ambayo ndiyo ilikuwa na idadi kubwa ya maambukizi ikishuhudia kushuka kwa kasi kwa maambukizi mapya ingawa maendeleo haya yanaweza kuwa ya muda mfupi, takwimu mpya kutoka kwa Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Ulimwenguni, WHO zimeonesha. 

Kutoka Maktaba: Abiria akiwa kwenye usafiri wa pikipiki maarufu kama Boda Boda mjini Kampaka nchini Uganda
© World Bank/Sarah Farhat

Ndoto za vijana Uganda zatishiwa na mlipuko mpya wa COVID-19

Shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni, WHO kanda ya Afrika hivi karibuni ilionya kuwa awamu ya pili ya janga la ugonjwa wa Corona au COVID-19 barani humo itakuwa shubiri siyo tu kijamii bali kiuchumi. Nchini Uganda hali hiyo sasa ni dhahiri kwa kuwa takwimu za afya nchini humo zinaonesha  ongezeko la mambukizi kutoka watu 200 mwezi Februari mwaka huu hadi wagonjwa zaidi ya 1,000 kwa siku mwezi Mei na kuilazimu serikali kutangaza maagizo mapya ya kuudhibiti.

Shughuli za ununuzi kwenye duka jijini Dar es Salaam, Tanzania wakati ugonjwa wa Corona ulivyoripotiwa Tanzania mwezi Machi mwaka huu.
UN News/ Stella Vuzo

Tanzania yashauriwa kujiunga na mpango wa chanjo wa COVAX 

Kamati iliyoundwa na Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kufanya tathmini juu ya Ugonjwa wa COVID-19 imependekeza taifa hilo kukubali Chanjo na kujiunga na COVAX ambao ni mkakati wa kimataifa wa kuhakikisha kila nchi inapata chanjo unaosimamiwa na shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO.  

Sven Torfinn/WHO 2016

Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO yazindua mkakati kutokomeza malaria katika nchi 25 ifikapo 2025 

Katika kuelekea  siku ya malaria duniani, inayoadhimishwa kila mwaka tarehe 25 Aprili,  shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO limepongeza idadi kubwa ya nchi zinazokaribia na kufikia, utokomezajhji kabisa wa malaria. Taarifa ya Jason Nyakundi inaeleza kwa kina.

Mpango mpya uliozinduliwana shirika hilo unakusudia kusitisha maambukizi ya ugonjwa huo katika nchi 25 zaidi ifikapo mwaka 2025. 

Sauti
3'36"
©UNHCR/Ruben Salgado Escudero

14 Aprili 2021

Takribani nusu ya wanawake wote katika nchi zinazoendelea, wananyimwa uhuru wao wa mwili, imesema ripoti ya UNFPA.

Kwa sababu ya COVID-19 Ramadhan mwaka huu itakuwa ngumu sana kwangu, anasema mkimbizi Anna anayeishi kwenye kambi ya wakimbizi ya Mbera nchini Mauritania.

Na FAO yatumia msemo wa tahadhari kabla ya hatari kunusuru mali na uhai Bangladesh.

Sauti
13'2"

12 Aprili 2021

Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO, kwa kushirikiana na mamlaka nchini Colombia wanatumia kila njia ikiwemo ya kutembea nyumba kwa nyumba ili kuwafikia watu wa jamii za asili walio katika mazingira magumu katika eneo la Amazon kusini mwa nchi ambao ni miongoni mwa makundi ya kipaumbele ya kupatiwa chanjo ya COVID-19.

 

Sauti
10'59"