Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au coronavirus">COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.
Taarifa kuhusu Virusi vya Corona
Apu za kwenye simu zachangia katika kudhibiti COVID-19- Dkt. Tedros
Mkurugenzi Mkuu wa shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO, Dkt. Tedros Ghebreyesus ametaja bara la Ulaya na Amerika kama maeneo ambako maambukizi mapya ya ugonjwa wa virusi vya Corona, au COVID-19 yameripotiwa kwa kiasi kikubwa, hususan katika siku nne zilizopita.
Mkimbizi atumia Yoga kuleta ustawi kwa wakimbizi wengine kambini Kakuma
Msongo wa mawazo, kiwewe na matatizo mengine ya akili ni moja ya changamoto zinazowapata wakimbizi kutokana na mazingira wanamoishi au maisha waliyopitia. Kutana na Rita Brown, mkimbizi kutoka Uganda ambaye anatumia nguvu ya mazoezi ya viungo aina ya Yoga kuleta ustawi na uponyaji kwa wakimbizi walioko katika kambi ya wakimbizi ya Kakuma nchini Kenya.
Siku ya Kimataifa ya Mtoto wa Kike: Fursa ya kuunda ulimwengu bora, mzuri na sawa kwa wasichana kila mahali.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres, kupitia ujumbe wake wa siku ya kimataifa ya mtoto wa kike anasema wasichana barubaru, na harakati za ulimwengu za mabadiliko wanazounda, ndio viongozi wapya wa wakati wetu.
Uzoefu wa UNAIDS katika VVU/UKIMWI watoa mwongozo wa kupunguza unyanyapaa wakati wa COVID-19
Kwa kutumia uzoefu wake wa miaka 40 ya kushughulikia ugonjwa wa UKIMWI, shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na masuala ya UKIMWI, UNAIDS, limetoa mwongozo mpya kuhusu jinsi ya kupunguza unyanyanyapaa na ubaguzi wakati wa kushughulikia COVID-19. Mwongozo huo unategemea ushahidi wa hivi karibuni juu ya kile kinachofanya kazi kupunguza unyanyapaa na ubaguzi unaohusiana na Virusi Vya UKIMWI, VVU na unatumika kwa COVID-19.
COVID-19 yashamirisha biashara mtandaoni:UNCTAD
Janga la corona au COVID-19 limebadili mtazamo wa watu kuhusu kuelekea zaidi kwenye ulimwengu wa kidijitali kwa mujibu wa matokeo ya utafidi wa wateja uliofanywa hivi karibuni ya shirika la Umoja wa Mataifa la biashara na maendeleo UNCTAD.
Gonjwa la COVID-19 limeumbua ukosefu wa maandalizi-Guterres
Miezi 9 tangu kusikia kwa mara ya kwanza kuhusu ugonjwa wa Corona au COVID-19, janga hilo tayari limeshasababisha vifo vya watu zaidi ya milioni moja miongoni mwa zaidi ya watu milioni 30 waliothibitika kuwa na ugonjwa huo katika nchi 190.
07 Oktoba 2020
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres leo amezindua tamko lake la kisera lenye mapendekezo matano ya kuchagiza mpango wa huduma ya afya kwa wote, UHC kwa lengo la kukabili vilivyo janga la COVID-19 hivi sasa pamoja na kuepusha majanga kama hayo siku za usoni.
WFP na serikali ya Nigeria kutoa msaada wa fedha taslimu na chakula kwa waathirika wa COVID-19.
Wataalamu wa afya TANZBATT 7 wapatiwa mafunzo dhidi ya COVID-19 nchini DR Congo.
Wataalamu wa afya TANZBATT 7 wapatiwa mafunzo dhidi ya COVID-19
Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC shughuli za ulinzi wa amani zinazofanywa na walinda amani wa Umoja wa Mataifa kutoka Tanzania wa kikosi cha 7, TANZBATT 7 cha kikosi cha kujibu mashambulizi FIB cha ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani MONUSCO zinaendelea sambamba na kuelimishana jinsi ya kujikinga na gonjwa la Corona au COVID-19 ambalo bado ni tisho duniani.Luteni Issa Mwakalambo, Afisa Habari wa TANZBATT 7 amefutilia mafunzo hayo na kutuandalia taarifa hii kutoka Beni jimboni Kivu Kaskazini.
Pikipiki za magurudumu matatu na mashua kutumika kusambaza chakula na pesa Nigeria
Shirika la mpango wa chakula la Umoja wa Mataifa WFP na serikali ya Nigeria wamezindua programu ya msaada wa chakula na fedha taslimu katika maeneo matatu ya mijini yaani Abuja, Kano na Lagos ambako kote huko ni kitovu cha COVID-19 nchini humo.
06 Oktoba 2020
Harakati za Umoja wa Mataifa za kutekeleza lengo namba 5 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs la usawa wa jinsia na uwezeshaji wanawake linaendelea kupigiwa chepuo na wadau mbalimbali likiwemo shirika la kiraia la Naserian wilayani Monduli mkoani Arusha nchini Tanzania.
Vita vinavyoendelea Mashariki mwa Ukraine vimeongeza madhila kwa maelfu ya wazee na sasa janga la corona au COVID-19 imekuwa ni kama msumari wa moto juu ya kidonda.
Kambale wageuka kichocheo cha uchumi kwa wanawake wa Ibadan Nigeria