Miji inapaswa kuwa kwenye moyo wa maendeleo endelevu-Antonio Guterres
Ufunguzi rasmi wa Kikao cha 10 cha Jukwaa la miji (WUF) umefanyika mjini Abu Dhabi,UEA leo jumapili, ambapo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres kupitia ujumbe wake wa video amewaambia wajumbe kuwa majiji na miji ni muhimu kuleta maendeleo endelevu kote ulimwenguni katika kipindi cha miaka kumi ijayo.