Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Abiria wakiwa wamejikinga na maambukizi ya mfumo wa hewa wakiwa katika treni za chini ya ardhi huko Shenzhen China
UN News/Jing Zhang

Virusi vya Corona sasa vyatangazwa kuwa dharura ya kiafya ya kimataifa

Mkutano wa pili wa kamati ya dharura ulioitishwa hii leo mjini Geneva Uswisi na shirika la afya duniani, WHO, chini ya sheria za kimataifa za afya (IHR) (2015) kuhusiana na mlipuko wa virusi vya corona 2019-nCoV nchini China, umeutangaza mlipuko huowa virusi vya corona kuwa ni dharura ya kiafya ya kimataifa, PHEIC.