Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Kinywa na meno yenye afya njema ni sehemu muhimu ya afya ya mtoto.
© WHO

Afya ya kinywa ni suala linaloendelea kupuuzwa licha ya madhara yake: WHO

Magonjwa ya kinywa, ingawa kwa kiasi kikubwa yanazuilika, husababisha mzigo mkubwa wa kiafya kwa nchi nyingi na huathiri watu katika maisha yao yote, na kusababisha maumivu, usumbufu, kulemaa na hata kifo kwa mujibu wa sjirika la afya la Umoja wa Mataifa duniani WHO huku ikikadiriwa kuwa magonjwa ya kinywa huathiri takriban watu bilioni 3.5 duniani kote.

Nasra Kibukila kutoka shirika la TEN/MET nchini Tanzania.
UN News/Anold Kayanda

Tunatamani  sheria ya elimu Tanzania itambue wasichana kuendelea na masomo baada ya ujauzito

Nasra Kibukila akiwakilisha Shirika la Mtandao wa Elimu Tanzania (TEN/MET) katika Mkutano wa 68 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake duniani ulioanza Machi 11 hadi Machi 22, 2024 jijini New York, Marekani amezungumza na Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa na kueleza wanayoyatekeleza nchini Tanzania ili kuhakikisha elimu bora hususani kwa wasichana.