Afya ya kinywa ni suala linaloendelea kupuuzwa licha ya madhara yake: WHO
Magonjwa ya kinywa, ingawa kwa kiasi kikubwa yanazuilika, husababisha mzigo mkubwa wa kiafya kwa nchi nyingi na huathiri watu katika maisha yao yote, na kusababisha maumivu, usumbufu, kulemaa na hata kifo kwa mujibu wa sjirika la afya la Umoja wa Mataifa duniani WHO huku ikikadiriwa kuwa magonjwa ya kinywa huathiri takriban watu bilioni 3.5 duniani kote.