'Hatuwezi kuwatelekeza watu wa Gaza': wakuu wa mashirika ya UN na mashirika yasiyo ya kiserikali
Wakati mapigano makali na mashambulizi ya makombora yaliendelea huko Khan Younis kusini mwa Gaza usiku wa kuamkia leo Jumatano, wasaidizi wakuu wa Umoja wa Mataifa na wakuu wa mashirika yasiyo ya kiserikali wameonya juu ya ‘matokeo mabaya’ ya kutofadhili shughuli za Shirika la Umoja wa Mataifa la msaada kwa wakimbizi wa Kipalestina UNRWA ambalo linashutumiwa kushirikiana na wanamgambo wa kipalestina wa Hamas.