Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Mwanamke akichota maji kutoka kwa chanzo kilichotengenezwa na UNICEF katika jimbo la Kasai, DR Congo.
© UNICEF/Gwenn Dubourthoumi

Habari kwa ufupi: Maji; Gaza; Saratani ya utotoni

Leo shirika la afya la Umoja wa Mataifa duniani limetoa muongozo mpya na nyenzo za kuboresha usambazaji mdogo wa maji. Mwongozo huo wa “ubora wa maji ya kunywa: usambazaji mdogo wa maji”, na vipengele vinavyohusiana vya ukaguzi wa usafi, unalenga kuboresha ubora wa maji hususan ya kunywa, kujenga utoaji wa huduma thabiti zaidi, na kupambana na kuongezeka kwa magonjwa katika jamii zilizo hatarini na zenye uhaba wa rasilimali hiyo muhimu.

Walinda amani wa Umoja wa Mataifa wakishika doria katika mji wa Goma mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo. (Maktaba)
MONUSCO/Kevin N. Jordan

DRC: UNHCR yahimiza ulinzi wa raia na upatikanaji wa njia salama za kufikisha misaada

Kufuatia ghasia zilizokithiri wiki iliyopita kati ya vikosi vya serikali na vikundi vya wanamgambo huko mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo -DRC, Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi- UNHCR limeeleza kusikitishwa na athari wanazozipata raia, wakiwemo takriban wakimbizi wa ndani 135,000 walioenda kusaka hifadhi katika mji wa Sake ulio karibu na jimbo la Goma. 

Naibu Mkurugenzi Mkuu wa FAO Beth Bechdol akitembelea Kituo cha Usambazaji wa Virutubisho vya Dharura vya Mifugo huko Isiolo, Kenya. (Maktaba)
FAO/Luis Tato

FAO yasihi wadau kuangalia mtindo mpya wa ufadhili

Takriban watu milioni 258 katika nchi na maeneo 58 ulimwenguni wanakabiliwa na njaa kali inayochochewa na migogoro ya silaha, majanga ya kiuchumi, mabadiliko ya tabianchi, umaskini na ukosefu wa usawa, limesema shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo FAO na kutaka wadau kuangalia upya mtindo wa ufadhili.

Sauti
2'40"
Mtoto wa mwaka mmoja anatibiwa utapiamlo katika Kituo cha Afya cha Abu Sunun nchini Sudan.
© UNICEF/Sara Awad

Hali si hali Sudan, msaada zaidi wahitajika: WHO

Nchini Sudan ambako kaimu mwakilishi wa shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO nchini humo Peter Graaff, akizungumza mjini Cairo Misri  hii leo kuhusu hali ya Sudan amesema miezi kumi ya vita imetumbukiza mamilioni ya watu katika janga lisiloelezeka la kibinadamu huku mapigano yakiendelea kusambaa katika maeneo mapya na kufurusha watu zaidi wengine mara kadhaa.