Habari kwa ufupi: Maji; Gaza; Saratani ya utotoni
Leo shirika la afya la Umoja wa Mataifa duniani limetoa muongozo mpya na nyenzo za kuboresha usambazaji mdogo wa maji. Mwongozo huo wa “ubora wa maji ya kunywa: usambazaji mdogo wa maji”, na vipengele vinavyohusiana vya ukaguzi wa usafi, unalenga kuboresha ubora wa maji hususan ya kunywa, kujenga utoaji wa huduma thabiti zaidi, na kupambana na kuongezeka kwa magonjwa katika jamii zilizo hatarini na zenye uhaba wa rasilimali hiyo muhimu.