Mafuriko ya ghafla Afghanistan ni tishio kubwa kwa watoto: UNICEF
Makumi ya maelfu ya watoto nchini Afghanistan wbado wameathiriwa na mafuriko yanayoendelea, hususan katika majimbo ya kaskazini ya Baghlan na Badakhshan na mkoa wa Ghor magharibi mwa Afghanistan, limesema leo shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia watoto UNICEF na kukumbusha kuwa mafuriko katika nchi hiyo ya Asia ya Kati yanasababisha tishio la haraka na la kudumu kwa watoto.