Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Viongozi wa mataifa, wafanyabiashara na mashirika ya kiraia walikusanyika mjini New York kwa ajili ya Mkutano wa Kilele wa Matarajio ya Hali ya Hewa ulioandaliwa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa.
© UN News/Anton Uspensky

Muungano wa mabadiliko ya tabianchi wadai hatua, huku Guterres akionya Ubinadamu umefungua milango ya kuzimu

"Joto la kupindukia linaleta madhara ya kutisha duniani ", kwa mujibu wa mkuu huyo wa Umoja wa Mataifa akizungumza leo katika mkutano wa kwanza kabisa wa ngazi ya juu wa matarajio kuhusu mabadiliko ya tabianchi mbele ya mbele ya muungano wa kimataifa wa kuchagiza hatua dhidi ya mabadiliko ya tabianchi ulijumuisha wachagizaji, watendaji, wanasiasa, wafanyabiashara, mashirika ya kimataifa na viongozi wa asasi za kiraia waliokusanyika New York kandoni mwa mjadala wa Baraza kuu UNGA78.

Rais wa Nigeria Bola Ahmed Tinubu wakati akihutubia katika mjadala Mkuu wa Mkutano wa 78 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa.
UN Photo/Laura Jarriel

Afrika ni ufunguo wa ulimwengu ujao - Rais Tinubu

“Afrika sio tatizo la kuepukwa na wala sio lakuonewa huruma. Afrika ni ufunguo wa ulimwengu ujao.” Ni kauli iliyotolewa na Rais wa Nigeria Bola Ahmed Tinubu wakati akihutubia katika mjadala Mkuu wa Mkutano wa 78 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa au UNGA78 jijini New York Marekani.