Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Watoto wakicheza kwenye moja ya kambi za wakimbizi wa ndani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC
© UNICEF/Gwenn Dubourthoumi

MONUSCO Bunia DRC watumia maigizo kuelimisha umma dhidi ya unyanyasaji wa kingono

Ili kudhibiti unyanyasaji wa kingono ambao wakati mwingine unafanywa na baadhi ya walinda amani wa Umoja wa Mataifa, huko jimboni Ituri katika mji wa Bunia nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo – MONUSCO wanatumia ubunifu wa sanaa za maigizo ya jukwaani kuelimisha umma

Sauti
1'43"
Mwanamke mjamzito mwenye umri wa miaka ishirini aliyezaliwa na virusi vya Ukimwi, hutumia dawa kuzuia maambukizi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto.
© UNICEF/UN0640796/Dejongh

Tunatekeleza ibara ya 5 ya Haki za binadamu kwa vitendo: UNFPA Kenya

Mkurugenzi Mkaazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Umoja wa Mataifa la afya ya uzazi na idadi ya watu UNFPA nchini Kenya Anders Tomsen, ameeleza shirika hilo linatekeleza ipasavyo tamko la Umoja wa Mataifa la haki za binadamu ambalo mwaka huu linafikisha miaka 75 hususan ibara ya Tano ambayo inasema Haki ya mtu ya kwamba asitumbukizwe kwenye vitendo vya mateso, ukatili, au adhabu dhalili.

Sauti
3'2"