UN na washirika wake watembelea kambi ya wakimbizi ya Jenin iliyoharibiwa vibaya
Maafisa wakuu wa Umoja wa Mataifa na washirika wafadhili Jumapili walitembelea kambi ya wakimbizi wa Kipalestina katika mji unaokaliwa wa Ukingo wa Magharibi wa Jenin, ambapo wameshuhudia uharibifu wa kushtua uliofanyika wakati wa uvamizi wa Israeli wiki hii iliyopita.