Guterres aziomba jumuiya za kimataifa kuwasaidie wananchi wa Haiti
Ulimwengu lazima uchukue hatua sasa kukomesha ghasia na ukosefu wa utulivu nchini Haiti, amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres hii leo wakati akitoa ombi la wadau wote kuchukuliwa hatua za haraka za kusaidia masuala ya kibinadamu, usalama na kisiasa.