Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Mwanamke akipokea dawa ya kuzuia malaria katika kituo cha afya nchini Uganda
© UNICEF/Maria Wamala

Nchi 12 Barani Afrika kuanza kutoa chanjo ya Malaria

Nchi 12 katika barani Afrika zinatazamiwa kupokea dozi milioni 18 za chanjo ya kwanza ya malaria katika kipindi cha miaka miwili ijayo imeeleza leo taarifa ya pamoja iliyotolewa na Mashirika ya Umoja wa Mataifa lile la Afya ulimwenguni WHO na linaloshughulika na watoto UNICEF huku wakishirikiana na Ubia wa chanjo duniani, GAVI. 

Kambi ya wakimbizi ya Jenin inapakana na manispaa ya Jenin na ndiyo kambi ya kaskazini kabisa katika Ukingo wa Magharibi.
© UNRWA/Dominiek Benoot

Ukingo wa Magharibi: UNICEF na OHCHR wakemea mashambulizi ya Israel mjini Jenin

"UNICEF ina wasiwasi mkubwa kutokana na kuongezeka kwa ghasia za hivi karibuni huko Jenin, katika Ukingo wa Magharibi.” Anasema Adele Khodr, Mkurugenzi wa UNICEF kanda ya Mashariki ya Kati na Afrika Kaskazini wakati Kamishna Mkuu wa Haki za Kibinadamu wa Umoja wa Mataifa Volker Türk akisema vurugu huzaa tu vurugu zaidi. Mauaji, kulemaza watu na uharibifu wa mali lazima vikomeshwe.