Guterres: Suriname msifanye maandamano ya vurugu
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ana wasiwasi na maandamano ya vurugu yaliyotokea nchini Suriname tarehe 17 mwezi huu wa Februari, 2023 ambapo majengo ya bunge yalivunjwa, mali ya watu binafsi kuharibiwa na watu wengi kujeruhiwa.