Malengo ya Maendeleo Endelevu yanaweza kufikiwa ‘licha ya nyakati zetu mbaya: Rais wa ECOSOC
Licha ya miaka miwili ya "mapambano ya kushangaza" dhidi ya janga la COVID-19, na huku kukiwa na changamoto zinazoongezeka za ulimwengu, matumaini ya kupatikana kwa maendeleo endelevu yanaendelea.” Amesema hii leo Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa la masuala ya Kiuchumi na Kijamii, ECOSOC, Collen Vixen Kelapile.