Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Wanafunzi wakihudhuria tukio baada ya masomo nchini Madagascar.
© UNICEF/Rindra Ramasomanana

Malengo ya Maendeleo Endelevu yanaweza kufikiwa ‘licha ya nyakati zetu mbaya: Rais wa ECOSOC 

Licha ya miaka miwili ya "mapambano ya kushangaza" dhidi ya janga la COVID-19, na huku kukiwa na changamoto zinazoongezeka za ulimwengu, matumaini ya kupatikana kwa maendeleo endelevu yanaendelea.” Amesema hii leo Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa la masuala ya Kiuchumi na Kijamii, ECOSOC, Collen Vixen Kelapile. 

Chanjo dhid ya homa ya Ini aina ya B Argentina
Photo: WHO/PAHO

WHO kuchunguza kuenea kwa homa kali ya ini isiyojulikana

Shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni, WHO limezindua utafiti duniani kote wenye lengo la kubaini idadi halisi na kiwango cha aina ya ugonjwa wa homa ya ini kali, Hepatitis miongoni mwa watoto, ambao ni tofauti na aina zote za homa ya ini zinazotambulika, wakati huu ambao ugonjwa huo umeripotiwa katika kanda 5 za WHO isipokuwa barani Afrika.

Sauti
2'20"
Vurugu za magenge mjni Port-au-Prince, Haiti, zinawatia hofu watu wazima na watoto vile vile.
UNDP Haiti/Borja Lopetegui Gonzalez

Licha ya vikwazo, WFP yaendelea kuokoa maisha Haiti 

Nchini Haiti, ambako karibu nusu ya idadi ya watu tayari hawana uhakika wa chakula, njaa inatazamiwa kuongezeka huku kukiwa na ongezeko la mfumuko wa bei, gharama kubwa za chakula na mafuta na kuzorota kwa usalama, linaonya Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani, WFP ingawa linaendelea kutoa msaada kwa Wahaiti walio katika mazingira hatarishi.

Sauti
2'30"
Wananchi wa kijiji cha Kuruwitu wakipakia matumbawe ya saruji kwenye boti tayari kwa kwenda kuyaweka katika eneo lililojitenga baharini.
UN/Thelma Mwadzaya

Matumbawe ya asili yaharibiwa, wanakijiji Kuruwitu waunda ya saruji na kuyaweka baharini

Maeneo ya ufukweni katika Kaunti ya Kilifi, Kenya yanavutia kwani ni tulivu na makazi ya viumbe mbalimbali. Matumbawe yana uhai na ni kiungo muhimu katika mfumo wa uhai kwenye mazingira ya baharini lakini katika baadhi ya maeneo kama Kuruwitu, kuna nyakati ambapo matumbawe yalikuwa hatarini kutoweka. Mwaka 2003 wakaazi wa Kuruwitu waliamua kuanzisha mpango wa kuimarisha hali ya bahari baada ya samaki kupungua na biashara ya matumbawe kuleta madhara. 

Walnda amani wa ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini DRC, MONUSCO wako chonjo kuhakikisha kuna usalama na hapa ni Djugu jimboni Ituru ambako walifika kuweka doria baada ya ripoti za kuweko kwa kikundi cha CODECO ambacho hushambulia raia.
MONUSCO/Force

Siku 5 za machungu kwa wakazi wa Lume, DRC: Watu 20 wauawa

Kutoka nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, MONUSCO umeripoti kuwa watu wapatao 20 wakiwemo watoto wawili wameuawa wakati wa mashambulizi yaliyofanywa na wafuasi wanaodaiwa kuwa wa kikundi kilichojihami cha Allied Democrait Forces, au ADF katika siku tano zilizopita huko eneo la Lume, jimboni Kivu Kaskazini.