Shambulio laua Watoto 14 nchini Syria
Takriban watoto 14 wameuawa na wengine kadhaa wamejeruhiwa katika shambulio lililotokea hii leo huko magharibi mwa Idlib kaskazini mashariki mwa Syria.
Takriban watoto 14 wameuawa na wengine kadhaa wamejeruhiwa katika shambulio lililotokea hii leo huko magharibi mwa Idlib kaskazini mashariki mwa Syria.
Hali ya usalama huko Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC inaendelea kuzorota ambapo shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR, linasema mauaji na uporaji wa mali za raia vinaendelea na kwamba kati ya mwezi Februari na mwezi uliopita wa Juni zaidi ya watu 800 wameuawa katika mashambulizi kutoka vikundi vilivyojihami.
Utafiti uliofanywa na shirika la kimataifa la nguvu za atomiki IAEA kuanzia mwezi Machi 2019 mpaka Aprili 2022 umegundua kuwa taratibu za kawaida za kufanya uchunguzi wa magonjwa ya moyo zimepungua kwa asilimia 64 duniani kote.
Katika kushughulikia mzozo wa vita ya Ukraine na Urusi ambayo imepandisha gharama mbalimbali za mazao na mbolea hii leo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amewasili jijini Instanbul nchini Uturuki kwa ajili ya kutafuta suluhu ya changamoto hizo.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amelaani shambulio la risasi lililotokea jana huko Zakho jimboni Dohuk katika mkoa wa Kurdish nchini Iraq na kusababisha vifo vya watu nane na wengine 23 kujeruhiwa.
Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo, FAO limeimarisha afya ya wakulima wa kaunti ya Migori. Hii ni baada ya kuzindua machi Mwaka huu mradi wa kilimo mbadala unaolenga kusitisha kile cha tumbaku. Kwa ushirikiano wa WHO na WFP, FAO inajivunia mafanikio kwani afya za wakulima wa Migori zimeimarika baada ya kuacha kilimo cha tumbaku na kukiongeza kipato chao.
wa Umoja wa Mataifa wa masuala ya kibinadamu nchini Cameroon, Olivier Beer ameeleza hofu yake juu ya athari za kufungwa kwa muda usiojulikana kwa hospitali ya Mada huko mkoa wa Far KAskazini nchini Cameroon baada ya shambulizi la tarehe Pili mwezi huu wa julai kutoka kundi la watu waliokuwa wamejihami.
Wakati Kenya inajiandaa kufanya uchaguzi mkuu tarehe 9 mwezi ujao wa Agosti, 2022 wataalamu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa wametoa wito kwa mamlaka nchini humo, wagombea nafasi za uongozi pamoja na vyama vya siasa kuimarisha mazingira wezeshi ili kuepuka ghasia na hatimaye uchaguzi huo ufanyike kwa amani.
Shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni, WHO kanda ya Afrika, limekaribisha uzinduzi uliofanywa na ubia wa chanjo duniani, GAVI wa fursa kwa nchi kuwasilisha maombi ya fedha ili kuanza kusambaza chanjo dhidi ya Malaria, hatua ambao WHO imesema itawezesha chanjo hiyo kufikia watoto walio hatarini zaidi kwa kuanzia na Ghana, Kenya na Malawi, ambazo tayari zilianza majaribio ya chanjo hiyo mwaka 2019 na hatimaye kusambazwa nchi zingine ambako Malaria imeota mizizi.
Hii leo katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York Marekani kumefanyika mkutano wa ngazi za juu maalum kuangazia masuala ya maendeleo barani Afrika.