Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Angela N'Habimana mwenye umri wa miaka 67 akiwa na mjukuu wake aitwaye Réponse kwenye kituo cha kijamii cha Kiwanja katika eneo la Rutshuru jimboni Kivu Kaskazini nchini DRC baada ya kukimbia mashambulizi kwenye makazi yao.
© UNHCR/Sanne Biesmans

Zaidi ya watu 800 wameuawa Mashariki mwa DRC kati ya Februari na Juni 2022- UNHCR

Hali ya usalama huko Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC inaendelea kuzorota ambapo shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR, linasema mauaji na uporaji wa mali za raia vinaendelea na kwamba kati ya mwezi Februari na mwezi uliopita wa Juni zaidi ya watu 800 wameuawa katika mashambulizi kutoka vikundi vilivyojihami.

Shamba la mmea wa tumbaku nchini Kenya
© WHO

FAO yawasaidia wakulima wa tumbaku Kenya, kuhamia katika mazao mbadala

Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo, FAO limeimarisha afya ya wakulima wa kaunti ya Migori. Hii ni baada ya kuzindua machi Mwaka huu mradi wa kilimo mbadala unaolenga kusitisha kile cha tumbaku. Kwa ushirikiano wa WHO na WFP, FAO inajivunia mafanikio kwani afya za wakulima wa Migori zimeimarika baada ya kuacha kilimo cha tumbaku na kukiongeza kipato chao.

Clara Magalasi kutoka maeneo ya kijijini ya mji mkuu wa Malawi, Lilongwe alitembea kilometa 4 kuhakikisha mtoto wake Grace mwenye umri wa miezi 22 anapata dozi yake ya nne na ya mwisho ya chanjo ya Malaria.
WHO Malawi

Mpango wa GAVI kuwezesha chanjo ya Malaria kupatikana zaidi Afrika- WHO

Shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni, WHO kanda ya Afrika, limekaribisha uzinduzi uliofanywa na ubia wa chanjo duniani, GAVI wa fursa kwa nchi kuwasilisha maombi ya fedha ili kuanza kusambaza chanjo dhidi ya Malaria, hatua ambao WHO imesema itawezesha chanjo hiyo kufikia watoto walio hatarini zaidi kwa kuanzia na Ghana, Kenya na Malawi, ambazo tayari zilianza majaribio ya chanjo hiyo mwaka 2019 na hatimaye kusambazwa nchi zingine ambako Malaria imeota mizizi.