Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Walinda amani wa Umoja wa Mataifa wakisindikiza wapiganaji wa M23 waliojisalimisha Kivu Kaskazini.
MONUSCO

DRC: Hali ya kawaida imerejea lakini bado tete

Kaimu Mkuu wa ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC Kassim Diagne amezungumza na waandishi wa habari kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa kwa njia ya video kutoka mji mkuu Kinshasa na kusema hali ya kawaida angalau imerejea lakini bado ni tete baada ya mamlaka kutoa wito kwa waandamanaji kusitisha vitendo hivyo sambamba na jeshi la serikali, FARDC kuimarisha usalama.

Muuguzi akifanya vipimo vya VVU katika Hospitali ya Wau, Sudan Kusini
© UNICEF/Albert Gonzalez Farran

Sasa utaweza kujipima mwenyewe VVU kwa dola 1  

Ushirikiano mpya uliotangazwa leo Julai 27 kati ya Clinton Health Access Initiative (CHAI) yaani mpango wa Clinton wa upatikaji Afya, MedAccess ambalo ni shirika linalolenga upatikanaji wa dawa kwa bei nafuu, na Kampuni ya Wondfo Biotech, utafanya uchunguzi wa Virusi Vya UKIMWI, VVU upatikane kwa dola 1 fedha za kimarekani kwa sekta ya umma katika nchi za kipato cha chini na cha kati, na hivyo kufanya kufanya kipimo hicho kuwa cha bei ya chini zaidi katika vipimo vyote vya kujipima VVU vilivyoidhinishwa na shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani, WHO. 

Walinda amani wakifanya doria huko Butembo, Kivu Kaskazini katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ili kuhakikisha usalama wa jamii.
UN Photo/Martine Perret

Shambulio dhidi ya walinda amani linaweza kuwa uhalifu wa kivita, walioshambulia MONUSCO wafikishwe kwenye sheria - Guterres 

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres amelaani vikali shambulio baya lililotokea jana tarehe 26 Julai huko Butembo, jimbo la Kivu Kaskazini dhidi ya askari wa kulinda amani wanaohudumu katika Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kuleta utulivu nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (MONUSCO).