Waafrika zaidi ya milioni 91 wanaishi na ugonjwa wa Homa ya Ini wakiwemo watoto chini ya miaka 5
Zaidi ya Waafrika milioni 91 wanaishi na Ugonjwa wa Homa ya Ini aina B au C, ambayo ni aina mbaya zaidi ya virusi, kulingana na chapisho lililotolewa Julai 27,2022 kwenye wavuti ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Ulimwenguni WHO.