Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Jengo la makazi ya watu likiteketea kwa moto baada ya kupigwa kombora kwenye mji mkuu wa Ukraine, Kyiv. Watu wawili walikufa na wengine 50 waliokolewa na wafanyakazi wa uokozi.
© UNDP Ukraine/Pavlo Petrov

Siku 100 za uvamizi wa Urusi nchini Ukraine: Vita ikome sasa- Guterres

Antonio Guterres, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ametoa taarifa yake hii leo jijini New York, Marekani kuhusu siku 100 za uvamizi wa Urusi huko Ukraine,  akisema kuwa vita hiyo tayari imesababisha vifo vya maelfu ya watu, uharibifu wa kupita kipimo, ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu usioelezeka na kuibua janga la pande tatu duniani: nishati, chakula na fedha, waathirikao zaidi ni watu walio hatarini, nchi na uchumi.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres (katikati) akizungumza katika  mkutano wa Stockholm +50 huko Sweden
© UNEP

Chonde chonde hebu tujikwamue kutoka kwenye janga hili la mazingira:UN 

Mkutano wa ngazi ya juu wa Umoja wa Mataifa kuhusu mazingira ya binadamu, Stockholm+50, umeanza leo kwenye mji mkuu wa Sweden, Stockholm kwa wito kutoka kwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres akizitaka nchi zote duniani kukumbatia haki za binadamu kwa ajili ya mazingira safi na yenye afya kwa wote hususan kwa jamii masikini, wanawake na wasichana, watu wa asili, vijana na vizazi vijavyo.