Shambulio lingine Mali dhidi ya walinda amani; 2 wauawa
Nchini Mali, walinda amani wawili wa Umoja wa Mataifa wanaohudumu kwenye ujumbe wa Umoja huo wa kulinda amani nchini humo, MINUSMA, wameuawa leo asubuhi kwenye mji wa Douentza ulioko mkoa wa Mopti kaskazini-mashariki mwa mji mkuu Bamako.