Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Kakuma, Kenya - 26 Machi, 2018: Wagonjwa wakiwa katika Duka la Dawa la Hospitali ya Misheni ya Kakuma. Hospitali hii ya Kaskazini mwa Kenya ni mojawapo ya vituo vichache katika eneo la Turkana ambapo wagonjwa wanaweza kupata ushauri wa ophthalmologic na u
WHO/Sebastian Liste through NOOR

Nilitamani kuwa muuguzi tangu ningali mdogo

Muuguzi Rebecca Deng ambaye ni mkimbizi wa Sudan Kusini anayeishi katika kambi ya wakimbizi ya Kakuma nchini Kenya ameisihi jamii kuhakikisha inapata elimu sahihi ya afya ya uzazi pamoja na kuhimiza wanawake na wasichana kutoacha kujiendeleza kielimu. 

Sauti
2'9"
Mifumo ya umwagiliaji maji inasaidia wakulima Uailili Timor Leste kuongeza mazao zaidi.
UNDP Timor-Leste

Kukabili changamoto za Afrika kunahitaji juhudi na kubadili mwelekeo:FAO

Kukabiliana na changamoto zinazoingiliana ambazo zinalikabili bara la Afrika na kutambua uwezo wake mkubwa kunahitaji juhudi za hali ya juu na kubadili mwelekeo kutumia njia mpya za kufanya kazi pamoja, amesema mkurugenzi mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo FAO QU Dongyu leo alipokuwa akifungua kikao cha 32 cha mkutano wa Kikanda wa Afrika (ARC32) wa shirika hilo la chakula na kilimo la Umoja wa Mataifa.

UNHCR na wadau wamehamisha wakimbizi kutoka Sudan na Sudan Kusini hadi mahali salama Ethiopia Benishangul ukanda wa Gumuz.
© UNHCR/Adelina Gomez Monteagud

Nani apewe nani anyimwe chakula: Uamuzi mgumu kwa mashirika ya UN 

Mamilioni ya familia za wakimbizi katika eneo la Mashariki mwa Afrika ziko hatarini kutumbukia kwenye njaa kali wakati huu ambapo mgao wa chakula unapungua kutokana na rasilimali za misaada ya kibinadamu kuzidiwa uwezo kwa sababu za mizozo lukuki, madhara ya tabianchi, janga la COVID-19 na ongezeko la bei ya chakula na mafuta, yamesema mashirika mawili ya Umoja wa Mataifa, lile la kuhudumia wakimbizi, UNHCR na mpango wa chakula duniani, WFP.