Kiwango cha maambukizi ya COVID-19 Afrika cha chini zaidi tangu April 2020
Maambukizi ya ugonjwa wa COVID-19 barani Afrika yamekuwa ni ya chini zaidi kuwahi kushuhudiwa tangu kuripotiwa kwa mara ya kwanza kwa mlipuko huo mwezi Aprili mwaka 2020, ambapo idadi ya wagonjwa walioripotiwa wiki 16 zilizopita imepungua sambamba na idadi ya vifo katika wiki 8 zilizopita.