Skip to main content
Karibu Umoja wa Mataifa
Lugha
  • العربية
  • 中文
  • English
  • Français
  • Русский
  • Español
  • Português
  • Kiswahili
  • Nyingine
    • Hindi हिंदी
    • duniani
Umoja wa Mataifa
Habari za UN
Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Search the United Nations

Tafuta Zaidi
  • Mwanzo
    • Afrika
    • Amerika
    • Asia Pasifiki
    • Mashariki ya Kati
    • Ulaya
  • Mada
    • Amani na Usalama
    • Ukuaji wa Kiuchumi
    • Msaada wa Kibinadamu
    • Tabianchi na mazingira
    • Haki za bindamu
    • Masuala ya UM
    • Wanawake
    • Sheria na Kuzuia Uhalifu
    • Afya
    • Utamaduni na Elimu
    • SDGs
    • Wahamiaji na Wakimbizi
  • Kwa kina
    • Habari kwa Picha
    • Mahojiano
    • Makala
    • Neno La Wiki
    • Makala Maalum
    • Videos
    • Siku za UN
  • Katibu Mkuu
    • Msemaji wa Katibu Mkuu
    • Taarifa zote
    • Hotuba muhimu
    • Mikutano na wanahabari
    • Safari za kikazi
  • Vyombo vya Habari
    • Video za Umoja wa Mataifa
    • Picha za Umoja wa Mataifa
    • Matukio ya Mikutanoni
    • Usajili kwa wanahabari
    • Webtv
  • Mwanzo
    • Afrika
    • Amerika
    • Asia Pasifiki
    • Mashariki ya Kati
    • Ulaya
  • Mada
    • Amani na Usalama
    • Ukuaji wa Kiuchumi
    • Msaada wa Kibinadamu
    • Tabianchi na mazingira
    • Haki za bindamu
    • Masuala ya UM
    • Wanawake
    • Sheria na Kuzuia Uhalifu
    • Afya
    • Utamaduni na Elimu
    • SDGs
    • Wahamiaji na Wakimbizi
  • Kwa kina
    • Habari kwa Picha
    • Mahojiano
    • Makala
    • Neno La Wiki
    • Makala Maalum
    • Videos
    • Siku za UN
  • Katibu Mkuu
    • Msemaji wa Katibu Mkuu
    • Taarifa zote
    • Hotuba muhimu
    • Mikutano na wanahabari
    • Safari za kikazi
  • Vyombo vya Habari
    • Video za Umoja wa Mataifa
    • Picha za Umoja wa Mataifa
    • Matukio ya Mikutanoni
    • Usajili kwa wanahabari
    • Webtv
 

Sajili

Kabrasha la Sauti

Kakuma, Kenya - 26 Machi, 2018: Wagonjwa wakiwa katika Duka la Dawa la Hospitali ya Misheni ya Kakuma. Hospitali hii ya Kaskazini mwa Kenya ni mojawapo ya vituo vichache katika eneo la Turkana ambapo wagonjwa wanaweza kupata ushauri wa ophthalmologic na upasuaji
WHO/Sebastian Liste through NOOR
Kakuma, Kenya - 26 Machi, 2018: Wagonjwa wakiwa katika Duka la Dawa la Hospitali ya Misheni ya Kakuma. Hospitali hii ya Kaskazini mwa Kenya ni mojawapo ya vituo vichache katika eneo la Turkana ambapo wagonjwa wanaweza kupata ushauri wa ophthalmologic na upasuaji

Nilitamani kuwa muuguzi tangu ningali mdogo

14 Aprili 2022
Afya

Muuguzi Rebecca Deng ambaye ni mkimbizi wa Sudan Kusini anayeishi katika kambi ya wakimbizi ya Kakuma nchini Kenya ameisihi jamii kuhakikisha inapata elimu sahihi ya afya ya uzazi pamoja na kuhimiza wanawake na wasichana kutoacha kujiendeleza kielimu. 

“Wakati nakua nilipenda kusema Lazima nifanye kazi hospitalini,” ndio inavyoanza video ya Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Wakimbizi UNHCR ikimuonesha Rebecca Deng ambaye ni muuguzi wa kujitolea wa shirika la Msalaba Mwekundu nchini Kenya. 

Deng ni mkimbizi wa Sudani Kusini anayeishi katika kambi ya wakimbizi ya Kakuma iliyoko nchini Kenya ambaye kupitia programu ya Uzazi salama inayofadhiliwa na UNHCR amekuwa akitoa elimu kwa wakimbizi wenzake kambini hapo. 

Anasema “ Nina furaha sana kuwasaidia watu, Jamii ilizoea kuniita iwapo kulikuwa na mjamzito aliyetaka kujifungua, walikuwa wanakuja kugonga mlango wangu nami nilivaa aproni yangu na kwenda mara moja.” 
Muuguzi huyu anaeleza jukumu lake hasa ni kuelimisha jamii na kuwaonesha faida za kwenda kujifungulia hospitalini. 

Anasema “ Unapojifungulia hospitalini hata kama tatizo linajitokeza daktari anaweza kulitatua. Na pia tunawaonesha jinsi ya kutunza ujauzito, kwa kuwa ukifuata vyema huduma za ujauzito daktari anaweza kuchukua vipimo vingi vya damu na kuweza kukuhudumia.” 

Pamoja na kuwapatia elimu, wajawazito pia wanapewa namba ya simu ya gari la wagonjwa iwapo watakuwa na dharura au wamepata uchungu ili waweze kupiga gari liwafuate kuwapeleka hospitali. 

Pichani iliyopigwa kutoka angani inaonyesha sehemu ya makazi kwenye kambi ya wakimbizi ya Kakuma nchini Kenya
Picha/Siegfried Modola
Pichani iliyopigwa kutoka angani inaonyesha sehemu ya makazi kwenye kambi ya wakimbizi ya Kakuma nchini Kenya

Lakini huduma hii muhimu ilisitishwa  kipindi cha janga la COVID-19, hawakuweza kutoa elimu na hali ilikuwa mbaya, wasichana wengi walipata ujauzito na hapa anatoa ushauri kwa wasichana. 

Anasema “ Ushauri wangu kwa wasichana kwanza waendelee na masomo, pili tunazungumza nao kuhusu ndoa katika umri mdogo. Tunasema waachwe kwanza waendelee na masomo. ...... Hata mimi mpaka sasa hivi naendelea na masomo .. Jioni najifunza lugha ya Kiingereza katika makazi ya wakimbizi.” 

Na mwisho ana ushauri kwa wanawake wote ... “ Tuendelee kuwaelimisha wanawake wajiendeleze kielimu, hakuna tofauti kati ya wanaume na wanawake, kazi inayofanywa na wanaume inaweza pia kufanywa na wasichana na wanawake.” 

 

♦ Kupata takwimu za waathirika vitani Ukraine bofya  hapa.
♦ Iwapo ungependa kupokea taarifa kutoka UN News Kiswahili kila wakati zinapochapishwa jisajili  hapa.
♦ Pia unaweza kupakua apu ili kusikiliza matangazo yetu wakati wowote popote ulipo.
♦ Tembelea pia chaneli yetu ya Youtube na pia Soundcloud na Twitter
COVID-19|Kambi ya Kakuma|Uzazi salama|kina mama wajawazito

SIKILIZA RADIO YA UMOJA WA MATAIFA

    Taarifa Zihusianazo

    Kambi ya wakimbizi ya Kakuma Kaskazini Magharibi mwa Kenyal.

    Mkimbizi atumia Yoga kuleta ustawi kwa wakimbizi wengine kambini Kakuma 

    Mkunga Adelaide Raul kutoka Msumbiji akifurahi na mama baada ya kumzalisha watoto mapacha

    Watoto milioni 116 kuzaliwa miezi 9 baada ya COVID-19 kutangazwa janga, je changamoto ni zipi?

    Mtoto mvulana akiwa pekupeku ambaye ndio amewasili tu kwenye kambi ya wakimbizi ya Kakuma Kaskazini Magharibi mwa Kenya kutokea Sudan Kusini akiwa na sanduku lake kichwani akijaribu kuwahi utaratibu wa kuandikisha wakimbizi

    Kakuma yawa mwenyeji wa jukwaa la kwanza la kimataifa la TEDx kwenye kambi ya wakimbizi:UNHCR

    Maktaba

    • Taarifa kwa watangazaji
    • Viunganishi vya Umoja wa Mataifa
    • Angalizo
    • UN Journal
    • Taarifa za Habari
    • Mikutano
    • Maktaba ya Picha na Video
    • Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu

    • Taarifa zote
    • Safari za kiofisi
    • Kona ya wanahabari
    • Kutoka Twitter ya Katibu Mkuu

    Msemaji wa UN

    • Nyaraka zote
    • Muhtasari wa mkutano na wanahabari
    • Maandishi ya mkutano na wanahabari
    • Taarifa kwa wanahabari

    Tupate

    • Facebook
    • Twitter
    • YouTube
    • RSS
    • Mawasiliano
    • Rambaza
    • Washirika wetu kwa sasa
    Umoja wa Mataifa
    Changia
    • Facebook
    • Twitter
    • YouTube
    • Soundcloud
    • Podcast
    • UN Social Media
    • A-Z Site Index
    • Hakimiliki
    • Maswali ya mara kwa Mara
    • Fraud Alert
    • Privacy Notice
    • Kanuni za matumizi
    • Facebook
    • Twitter
    • YouTube
    • SoundCloud
    • Podcast
    • More Socials