Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Mama na mwanae wakiondoka kituo cha treni cha Lvivi nchini Ukraine.
© UNICEF/Giovanni Diffidenti

Mtu 1 kati ya 6 ni mkimbizi wa ndani Ukraine:IOM

Ripoti mpya iliyotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la uhamiaji IOM inasema mtu 1 kati ya 6 ni mkimbizi wa ndani nchini  Ukraine na hivyo kuifanya idadi ya watu waliokimbia makazi yao na kusalia wakimbizi wa ndani tangu kuanza kwa mzozo wa Ukraine tarehe 24 mwezi Februari mwaka huu kufikia zaidi ya watu milioni 7.7 sawa na asilimia 17 ya watu wote wa taifa hilo.

Sauti
1'59"
Mwanzilishi mwenza na Mkurugenzi wa Tai (Tai Tanzania na Tai Plus)
Ian Tarimo/Tai Tanzania

Tai Tanzania, taasisi inayotambuliwa na mashirika ya UN kwa kuleta mabadiliko chanya Tanzania

Taasisi hiyo inayofahamika kwa jina la Tai, katika miaka ya hivi karibuni imefanikiwa kuungwa mkono na mashirika ya Umoja wa Mataifa lilikwemo la kuhudumia watoto, UNICEF, na pia shirika la idadi ya watu na afya ya uzazi, UNFPA ambapo mradi na UNICEF ulihusu usafi wakati wa hedhi na wa UNFPA ukiangazia unyanyasaji wa kijinsia na ndoa za utotoni. 

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António  Guterres akizungumza na wanahabari jijini New York, Marekani mbele ya bunduki iliyokunjwa inayoashiria usalama au bila mapigano.
UN /Eskinder Debebe

Pasaka ya waothodoksi Ukraine na Urusi ikikaribia, sitisheni mapigano kwa siku 4: Guterres

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametoa wito wa siku nne za sitisho la mashambulizi nchini Ukraine kuanzia Alhamisi ya wikii hii wakati huu ambapo wiki takatifu ya kuelekea sikukuu ya PAsaka kwa waumini wa madhehebu ya kikristo ya kiothodoksi nchini Ukraine ikianza keshokutwa Alhamisi. Ametaka sitisho hilo liendelee hadi Jumapili tarehe 24 mwezi huu kilele cha Pasaka ya kiothodoksi.

Akarurimana James ni mkimbizi kutoka Burundi ambaye amenufaika na ardhi iliyotolewa na serikali ya DRC kwa ajili ya wakimbizi na wenyeji wao kwa lengo la kuimarisha kujitegemea.
UN/Byobe Malenga

Wakimbizi wa Burundi nchini DRC washukuru kupatiwa ardhi ya kilimo

Nchini Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo DRC, serikali imetangaza kutenga ekari  500 za ardhi kwa ajili ya kilimo itakayotumiwa na wakimbizi kutoka Burundi pamoja na wenyeji, kwa lengo la kuimarisha hali ya kujitegemea na kuishi pamoja kwa amani. Kwa kiasi kikubwa wakimbizi hao wamekuwa wakitegemea msaada kutoka shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR na jamii za wenyeji zinazowahifadhi wakimbizi hao.  

Sauti
2'12"