Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Maelfu ya familia wamehama makazi yao kutokana na ukame wa hivi karibuni nchini Ethiopia
© UNHCR/Eugene Sibomana

Waziri wa mambo ya nje wa Uingereza atembelea waathirika wa ukame Ethiopia atoa ahadi ya kuendelea ushirikiano na UN

Waziri wa Mambo ya Nje wa Uingereza, James Cleverly akiambatana na Mwakilishi wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF Ethiopia, Gianfranco Rotigliano wametembelea eneo la Afar, nchini Ethiopia kujionea athari za ukame kwa watoto na familia na kutathimini hatua za dharura zizazochukuliwa na UNICEF ambapo Uingereza ni mdau muhimu kama mwanachama wa Umoja wa Mataifa na muhisani.

Sauti
2'12"
Mwanamke aliyezaliwa na VVU akipokea dawa kwenye kliniki nchini Burkina Faso
© UNICEF/Frank Dejongh

Ili kuumaliza UKIMWI lazima tuweke usawa duniani kote – Katibu Mkuu UN

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres kupitia ujumbe wake wa Siku ya UKIMWI Duniani, siku ambayo huadhimishwa kila mwaka tarehe Mosi Desemba, amesema ili kuumaliza ugonjwa huo lazima kwanza kukomesha ukosefu wa usawa ambao unakwaza hatua za kusonga mbele katika mapambano dhidi ya ugonjwa huu unaohatarisha maisha ya watu ulimwenguni kote.

Wanawake katika kambi ya Dadaab nchini Kenya
UN Women

Wanawake Dadaab Kenya wajumuika kukabili misimamo mikali

Nchini Kenya shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na masuala ya wanawake, UN Women kwa ushirikiano na wadau wanajengea uwezo wajenzi wa amani mashinani hata kwenye maeneo yenye changamoto kama vile kambi ya wakimbizi ya Daadab kwenye kaunti ya Garissa nchini humo kwa lengo la kuepusha vijana kutumbukizwa kwenye vikundi vyenye msimamo mkali.

Sauti
2'15"
Ina Maria Shikongo, mwanaharakati wa watu wa jamii ya asili kutoka Namibia akiwa kwenye maandamano huko COP27 Sharm-el-Sheikh nchini Misri.
UN News/Laura Quinones

Wanaharakati huko COP27 wasema hakuna hatua kwa tabianchi bila kujali haki za binadamu

Huko Sharm-el-Sheikh nchini Misri, kwenye mkutano wa 27 wa nchi wanachama wa Mkataba wa mabadiliko ya tabianchi, COP27, tarehe 17 mwezi huu wa Novemba yalishuhudiwa maandamano ya maelfu ya wawakilishi wa watu wa jamii ya asili, wanawake, wanarahakati wa masuala ya jinsia, vijana, mazingira na haki kwa tabianchi kutoka pande mbalimbali za dunia.

Sauti
3'51"
Michael Dunford, Mkurugenzi wa WFP Pembe ya Afrika akihojiwa na UN News.
UN/ Leah Mushi

Hatari ya baa la njaa bado ni jinamizi linaloizonga Somalia: WFP Dunford

Ukame uliolighubika eneo la Pembe ya Afrika kwa miongo minne mfululizo umesababisha changamoto kubwa kwa mamilioni ya raia wa Kenya, Ethiopia na Somalia nchi ambayo maeneo mengi yanakabiliwa na kutokuwa na uhakika wa chakula na hatihati ya kutumbukia kwenye baa la njaa. Mashirika ya misaada ya kibinadamu likiwepo la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani WFP yako mstari wa mbele kuwasaidia watu wenye uhitaji hususani wa chakula.

Sauti
2'