Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Watoto wakiteka maji machafu katika mto karibu na nyumbani jimbo la Ruyigi nchini Burundi. Septemba 14, 2017
© UNICEF/UN0185046/Haro

Licha ya ahadi, Burundi yaendelea kukiuka haki za binadamu na kufunga malngo wa demokrasia: HRC

Tume ya Umoja wa Mataifa ya uchunguzi kuhusu hali ya haki za binadamu nchini Burundi imesema licha ya ahadi za awali za Rais Évariste Ndayishimiye za kuboresha haki za binadamu nchini mwake na kurejesha utawala wa sheria, bado hakuna hatua zozote zilizochukuliwa kutimiza ahadi hizo, huku jukwaa la kidemokrasia likiendelea kufungwa na ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu ukitamalaki tangu Rais huyo achukue madaraka Juni 2020.

Sauti
3'32"
Mwanafunzi mwenye uoni hafifu akifanya mazoezi ya kutumia mashine ya nukta nundu kwenye shule ya watu wasioona ya Al-Noor  huko Mogadishu nchini Somalia.
UN Photo/Ilyas Ahmed)

MINUSCA yafanikisha wasichana bubu na viziwi kujikwamua

Msichana Theresa Kpana nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR ambaye ni bubu na kiziwi baada ya kushindwa kuendelea na masomo ya elimu ya juu kutokana na ukosefu wa miundombinu kwa watu kama yeye, sasa amechukua hatua ya kuunda kikundi cha wasichana 60  viziwi na bubu ili hatimaye wapate stadi za maisha na haki zao zilindwe kwa kuwa hivi sasa mustakabali wao uko mashakani.

Sauti
2'22"
Mfanyakazi wa ndani kutoka  makazi ya Kalayanpur nchini Bangladesh amepoteza kazi sababu ya janga la COVID-19
WFP/Sayed Asif Mahmud

WHO inachunguza hatari za maambukizi ya COVID-19 kwa watoto na barubaru

Wakati idadi ya wagonjwa wa corona au COVID-19 waliothibitishwa au kukutwa na virusi miongoni mwa watoto imefikiwa kiwango ambacho hakijawahi kushuhudiwa tangu kuzuka kwa janga hilo na tangu kuanza kwa muhula mpya wa masomo katika nchi mbalimbali, shirika la afya duniani WHO linaamini kuwa aina mpya ya virusi vya Corona inaonekana kuwagusa zaidi vbarubaru. 

Mikoko inasadia kutunz mazingira ambayo husaidia mazao ya baharini kuwa na faida
Manglar Vivo Project, UNDP Cuba

Mradi wa kuhifadhi mikoko Senegal waongeza pia kipato cha wavuvi wa chaza

Nchini Senegal, mradi wa pamoja wa mfuko wa Umoja wa Mataifa wa maendeleo ya kilimo duniani, IFAD na serikali ya taifa hilo la Afrika Magharibi umesaidia kurejeshwa upya kwa maelfu ya hekta za mikoko baharini na hivyo kusaidia jamii za wavuvi kuinua kipato chao na wakati huo huo kuwa na  mnepo dhidi ya mabadiliko ya tabianchi.

Sauti
3'6"
Chanjo
Janssen

Tambueni chanjo zote za COVID-19 zilizoidhinishwa na WHO

Mkurugenzi Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni, WHO, Dkt. Tedros Ghebreyesus ametaka nchi zote duniani kutambua chanjo zilizoidhinishwa na shirika hilo kwa matumizi ya dharura dhidi ya ugonjwa wa Corona au COVID-19 wakati huu ambapo bado kuna pengo kubwa la utoaji wa chanjo hiyo katika maeneo mbalimbali duniani hususan barani Afrika.