Licha ya ahadi, Burundi yaendelea kukiuka haki za binadamu na kufunga malngo wa demokrasia: HRC
Tume ya Umoja wa Mataifa ya uchunguzi kuhusu hali ya haki za binadamu nchini Burundi imesema licha ya ahadi za awali za Rais Évariste Ndayishimiye za kuboresha haki za binadamu nchini mwake na kurejesha utawala wa sheria, bado hakuna hatua zozote zilizochukuliwa kutimiza ahadi hizo, huku jukwaa la kidemokrasia likiendelea kufungwa na ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu ukitamalaki tangu Rais huyo achukue madaraka Juni 2020.